Wanamichezo wa MSD Watoa Msaada wa Kijamii Kituo cha Afya Ngamiani
Wanamichezo wa Bohari ya Dawa (MSD) wanaoshiriki kwenye mashindano ya SHIMUTA 2024 mkoani Tanga wametumia siku ya leo ya mapumziko kutembelea Kituo cha afya Ngamiani kilichopo mkoani Tanga na kutoa msaada wa bidhaa za afya kwa Wodi ya mama na mtoto.