BOHARI YA DAWA ( MSD) IMEINGIA MAKUBALIANO NA JESHI LA POLISI TANZANIA
Bohari ya Dawa ( MSD) imeingia makubaliano na Jeshi la Polisi Tanzania yanayolenga kuimarisha ulinzi na usalama wa bidhaa za afya zinazosambazwa na MSD nchini. Makubaliano hayo pia yamelenga kusimamia kikamilifu mfumo wa usafirishaji wa bidhaa za afya na hivyo kuufanya kuwa salama na kuhakikisha bidhaa za afya zinafika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya zikiwa salama.
Akizungumza kwenye tukio la kutia saini makubaliano hayo Kamishina wa Oparesheni na mafunzo wa Jeshi la Polisi, Awadhi Juma Haji, amesema Makubaliano haya ni hatua muhimu katika kuimarisha usimamizi wa usafirishaji wa bidhaa za afya, lakini pia kufunga mianya ya uharibifu na wizi wa mali. “Hii ni hatua kubwa na sisi kama jeshi la polisi tutahakikisha kazi hii inafanyika kikamilifu kwakuwa bidhaa zinazosambazwa na MSD ni mali ya serikali na mnufaika mkuu ni mwananchi hivyo zinapaswa kulindwa kikamilifu aliongeza ndugu Haji”.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Mavere Tukai amesema kutokana na kukua na kupanuka kwa majukumu ya MSD kuna umuhimu wa kuimarisha mahusiano na jeshi la polisi kwenye majukumu mbalimbali yanayofanywa na MSD. “Tunategemea ushirikiano huu wa Jeshi la Polisi na MSD utakwenda kudhibiti mianya yote ya upotevu wa bidhaa za afya na kuhakikisha usalama wa dawa zinazohitajika kwa afya ya Watanzania.
- Log in to post comments