Skip to main content

MSD YATUNUKIWA TUZO YA UMAHIRI WA UTOAJI HUDUMA

Bohari ya Dawa (MSD), imetunukiwa tuzo ya umahiri wa utoaji huduma kwenye sekta ya Famasi nchini (Award of Service Excellence in Pharmaceutical Sector) kupitia tuzo za mwaka za Tanzania Service Excellence Award 2024, zilizoandaliwa na taasisi ya Charted Institute of Customer Service (CICM) Tunzo hizo zimetolewa hapo jana na taasisi hiyo katika hafla maalum iliyofanyika katika ukumbi wa Holiday In, jijini Dar es Salaam 

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Kaimu Meneja wa Huduma kwa Wateja wa MSD Gendi Machumani amesema kupata tuzo ya utoaji huduma bora katika sekta ya afya inaonyesha jinsi jamii inavyothamini huduma bora zinazotolewa na MSD. Hatua hii inadhihirisha  mabadiliko makubwa ya kitaasisi chini ya Mkurugenzi Mkuu Mavere Tukai, ambapo taasisi imeweza kufanya kazi kwa ufanisi na kutimiza malengo ya kuhakikisha tunaboresha mnyonyoro wa ugavi wa bidhaa za afya nchini.

Ameongeza kuwa tuzo hii  inawafanya kuendelea kuwajibika kwa ufanisi na kuhakikisha afya za Watanzania zinalindwa  kwa kupeleka bidhaa za afya zenye ubora na gharama nafuu na kwa wakati.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.