Skip to main content
  • MSD Yashiriki Michuano ya SHIMUTA 2024

    Wachezaji wa Bohari ya Dawa (MSD) watakaoshiriki kwenye mashindano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma,Taasisi na Makampuni Binafsi (SHIMUTA)  mwaka 2024 jijiniTanga, leo Ijumaa tarehe 8 Novemba 2024 wameagwa na Menejimenti ya MSD na kuanza safari ya kuelekea kwenye mashindano hayo. 

    Akizungumza wakati wa kuwaaga wachezaji hao Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Elisamehe Macha amewakumbusha watumishi hao kuwa michezo ni sehemu ya kazi hivyo wanapaswa kuhakikisha wanaenzi tunu za MSD ikiwemo uhodari na nidhamu kama wanapokuwa sehemu zao za kazi. 

  • Watumishi wa MSD Wajengewa Uwezo, Juu ya Mifumo ya Usimamizi Ubora

    Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wanaosimamia mifumo ya Usimamizi wa Ubora  (QMS) wamejengewa uwezo ili kutekeleza na kusimamia majukumu yao kwa ufanisi na weledi kazinini.

    Akimzungumza wakati wa kufunga Mafunzo hayo, Kaimu Meneja wa Udhibiti Ubora wa MSD, Bi. Estella Meena alisema mafunzo hayo maalum yanatarajiwa kuwa chachu kuhakikisha matakwa ya ithibati ya Ubora wa kimataifa, yaani  ISO 9001:2015 yanatekelezwa kikamilifu, hivyo kuboresha utendaji na kuhakikisha malengo ya taasisi yanafikiwa.

  • MSD na CRDB Wabadilishana Uzoefu

    Katika hatua ya kuongeza ujuzi katika utoaji wa huduma kwa wateja Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wa Kurugenzi ya Ugavi wanaofanya kazi kwenye Idara ya Huduma kwa Wateja wametembelea Ofisi za Makao Makuu ya Benki ya CRDB zilizopo jijini Dar es Salaam. 

    Lengo la ziara hiyo ni kubadilishana uzoefu na kujifunza namna Benki hiyo inavyotoa huduma kwa wateja wake na namna inavyoweza kusimamia na kutatua malalamiko ya wateja. 

  • MSD Yashiriki Shughuli za Kijamii na Kutembelea Wateja Wake, Ikiadhimisha Miaka 30 ya Utendaji Toka Ianzishwe

    Katika maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Wateja kwa mwaka huu 2024, ambayo yalienda sambamba na sambamba na shughuli za kuadhimisha miaka 30 ya MSD, jumla ya wateja 18 walitembelewa kupitia kanda zote za MSD na kujadiliana masuala mbalimbali ya kuboresha huduma zinazotolewa na MSD pamoja na mahusiano na ushirikiano na wateja.

  • Mganga Mkuu Mkoa wa Pwani, Apongeza Ushirikiano Baina ya MSD na Wateja Wake.

    Bohari ya Dawa(MSD) Kanda ya Dar es Salaam imeandaa kikao kazi na wadau wake wa mkoa wa Pwani kilichofanyika Mkoani Pwani - Wilayani Kabaha katika Chuo cha Mwalimu Nyerere  kuzungumza kwa pamoja namna ya koboresha upatikanaji wa bidhaa za afya.

    Akizungumza kwenye kikao hicho Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Dkt. Urio Kusirye amesema vikao kazi hivyo ni muhimu kwani vinachangia kuhakikisha huduma za afya ndani ya Mkoa wa Pwani zinakuwa endelevu na bora.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.