MSD KUSAMBAZA VIDONGE MIL. 22 VYA VITAMINI A NCHINI
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameikabidhi Serikali ya Tanzania kupitia kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel kwa niaba ya Waziri ya Afya Mhe. Ummy Mwalimu vidonge milion 22 vya matone vya Vitamini A kwa ajili ya watoto, vilivyotolewa na serikali ya Canada, kupitia shirika la Nutrition International (NI).
Dkt. Kikwete, amekabidhi dawa hizo akiwa mmoja wa wajumbe wa bodi wa Shirika la kimataifa la Nutrition international ambalo ndio limetoa msaada huo.