Skip to main content
  • MSD Kilimanjaro Yajadili Mbinu Kuboresha Uhusiano na Huduma kwa Wateja

    ARUSHA.

    MSD Kanda ya Kilimanjaro imekutana na wateja wake wanaopata huduma kutoka Kanda hiyo ambao ni kutoka mikoa yaArusha, Kilimanjaro na Manyara, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanagusa pande hizo, kwa lengo la kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi. 

    Mkutano huo wa siku moja umefanyika Mkoani Arusha ukiwa na lengo la kujenga uhusiano mzuri baina ya MSD Kanda ya Kilimanjaro na wateja wake wote wanaohudumiwa na Kanda hiyo.

  • MSD Kanda ya Mbeya, Yateta na Wafamasia Kuboresha Huduma

    MBEYA:

    MSD Kanda ya Mbeya imefanya kikao na wafamasia kutoka halimshauri 17 na wafamasia wa mikoa yote inayohudumiwa na Kanda hiyo

    Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya Bw. Marco Masala amesema lengo la kikao hicho ni kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za upatikanaji wa bidhaa za afya katika mikoa hiyo, pamoja na kuimarisha uhusiano.

    Pamoja na mambo mengine kupitia kikao hicho wamekubaliana kuunda kamati maalum ya kudumu itakayosaidiana na Kanda ya MSD Mbeya kufuatilia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa kwenye kikao hicho. 

  • Kamati ya CCM Mkoa wa Njombe, Yatembelea Kiwanda cha MSD- Idofi

    NJOMBE

    Kamati ya CCM Mkoa wa Njombe ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe.Deo Sanga, Mbunge wa jimbo la Makambako, imetembelea na kukagua maendeleo ya Mradi wa Kiwanda cha mipira ya mikono, kilichoko Idofi Makambako.

    Kamati hiyo iliyoongozana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka imeelezea kufurahishwa na hatua zilifikiwa katika ujenzi wa mradi huo na kuipongeza Menejimenti na Wataalamu wa MSD kwa kufanikisha ujenzi huo.

  • MSD Yafuatilia Ubora wa Dawa-Vituoni

    Bohari ya dawa (MSD) kupitia Kitengo chake cha Udhibiti Ubora imeendelea na zoezi la ufuatiliaji wa ubora wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ambavyo vimeshasambazwa kwa wateja ili kuhakikisha bidhaa hizo za afya hasa dawa, zinaendelea kuwa na ubora unaotakiwa.

  • MSD Yaboresha Huduma za Kusafisha Damu- Hospitali ya Tumbi

    PWANI

    Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani - Tumbi imeanza kutoa huduma mpya ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo. Huduma hii imeanza kutolewa baada ya Bohari ya dawa (MSD) kukamilisha usimikaji wa  mashine za kisasa 10 za kusafisha damu, baada ya hospitali ya rufaa ya Tumbi kuboresha miundombinu ya kuwezesha huduma hiyo kupatikana.

    Hatua hiyo ni muendelezo wa maboresho ya huduma za afya nchini yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Afya.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.