MSD Yasambaza Vifaa Tiba vya Kisasa Wilayani Mafia
BOHARI ya Dawa (MSD) imesema usambazaji wa dawa na vifaa vya kisasa Kisiwani Mafia mkoani Pwani umefanikiwa kupunguza rufaa za wagonjwa kutoka kisiwani humo kwenda kutibiwa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana kisiwani Mafia Afisa Huduma kwa Wataeja wa MSD wa kanda hiyo Diana Kimario, alisema Bohari hiyo imefanikiwa kupunguza rufaa za wagonjwa kutoka kisiwani Mafia kwenda jijini Dar es Salaam kwa kufunga vifaa tiba vya kisasa hususani vya maabara na upasuaji.