Skip to main content
  • MSD Yaja na Mpango Kabambe Kuhudumia Wateja Wakubwa (Corporate Customers)

    Bohari ya Dawa (MSD) imekutana na wateja wake Wakubwa(Corporate Customers) wanaohudumiwa na Kanda ya MSD Dodoma, kujadiliana na kuweka mikakati ya pamoja ya kuimarisha na kuboresha upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za afya kwa ajili ya huduma maalum zinazotolewa na wateja hao.

  • MAFANIKIO YA MSD KATIOKA MIAKA MINNE YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    UPATIKANAJI WA BIDHAA ZA AFYA

    Bohari ya Dawa imeendelea kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya katika vituo vya kutolea huduma za afya. Uwepo wa bidhaa za afya umekuwa ukipimwa kwa bidhaa za afya ashiria 290 lakini kutokana na kuimarishwa mifumo ya utoaji huduma na nia ya Serikali kuboresha maisha ya Watanzania kuanzia mwaka wa fedha 2023/24, idadi ya bidhaa ashiria zinazotumika kupima hali ya upimaji wa bidhaa za afya zimeongezeka kutoka bidhaa 290 hadi kufikia bidhaa 382.

  • MSD MBEYA, YAJADILIANA NA WADAU WAKE KUIMARISHA HUDUMA 

    Wateja wa MSD kutoka mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa, na halmashauri ya Makete Wahimizwa kutumia vyanzo vingine vya mapato kununua bidhaa za afya kutoka Bohari ya Dawa (MSD).

    Aidha wametakiwa kulipa au kupunguza madeni yao wanayodaiwa na MSD ili kuipa nguvu ya kiuchumi katika mzunguko wa ugavi wa bidhaa za afya, badala ya kurundika madeni yao.

  • Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) yatembelea MSD

    Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.

  • MSD YAKABIDHI JENERETA LA KVA 75 KWA HOSPITALI YA WILAYA YA KITETO

    Hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto mkoani Manyara imeondokana na changamoto ya kukatiza baadhi ya huduma za matibabu kama upasuaji na pindi umeme unapokatika baada ya Bohari kuu ya dawa MSD kukabidhi jenereta lenye thamani ya shilingi milioni 65 itakayotumika kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano mjini Kibaya wilayani Kiteto, meneja wa MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amesema jenereta hilo lenye uwezo wa KVA 75 ni sehemu ya mahitaji ya vifaa vya afya vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 699 vilivyoagizwa na hospitali hi

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.