Skip to main content
  • MSD yafanya kikao na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC),

    Bohari ya Dawa (MSD) leo imefanya kikao muhimu na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Mheshimiwa Elias M. Magosi, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa SADC, kikao hiko kiliongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, kilikuwa na lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya afya.

    Katika kikao hicho, pande zote mbili zilijadiliana kuhusu mikakati ya pamoja ya kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya ndani ya ukanda wa SADC, kuongeza usalama wa bidhaa za afya, pamoja na kushirikiana katika maeneo ya uzalishaji, utafiti, na usambazaji wa dawa.

  • Msd yatunukiwa tuzo kwa kuwezesha matibabu ya moyo nchini

    Bohari ya Dawa (MSD) imetunukiwa tuzo maalum na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kutambua mchango na ushirikiano wake katika kuboresha huduma na matibabu ya Programu za Moyo nchini. 

    Tuzo hiyo maalum, imekabidhiwa na Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Nassor Ahmed Mazrui, wakati akifunga mkutano wa siku tatu wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo, ulioandaliwa na taasisi hiyo ya JKCI, na kukutanisha Wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi, madaktari, watafiti, wasambazaji Dawa na Vifaa tibawa visiwani humo.

  • MSD na JKCI Kuimarisha Ushirikiano wa Kimkakati Kuboresha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya.

    #Zanzibar,

    Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Mavere Tukai, amebainisha kwamba Bohari ya Dawa kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), wanaendelea kuimarisha ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini.

  • MSD YATUNUKIWA TUZO YA UMAHIRI WA UTOAJI HUDUMA

    Bohari ya Dawa (MSD), imetunukiwa tuzo ya umahiri wa utoaji huduma kwenye sekta ya Famasi nchini (Award of Service Excellence in Pharmaceutical Sector) kupitia tuzo za mwaka za Tanzania Service Excellence Award 2024, zilizoandaliwa na taasisi ya Charted Institute of Customer Service (CICM) Tunzo hizo zimetolewa hapo jana na taasisi hiyo katika hafla maalum iliyofanyika katika ukumbi wa Holiday In, jijini Dar es Salaam 

  • BOHARI YA DAWA ( MSD) IMEINGIA MAKUBALIANO NA JESHI LA POLISI TANZANIA

    Bohari ya Dawa ( MSD) imeingia makubaliano na Jeshi la Polisi Tanzania yanayolenga  kuimarisha ulinzi na usalama wa bidhaa za afya zinazosambazwa na MSD nchini. Makubaliano hayo pia yamelenga kusimamia kikamilifu mfumo wa usafirishaji wa bidhaa za afya na hivyo kuufanya kuwa salama na kuhakikisha bidhaa za afya zinafika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya zikiwa salama.  

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.