Katibu Mkuu Afya, Aitaka MSD Kuwajali Wateja Wake
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. John Jingu ameilekeza Bohari ya Dawa (MSD) kuwajali wateja na kuwashirikisha katika suala zima la kuwapa huduma za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za Afya nchini.
Dkt. Jingu amesema hayo wakati akifungua kikao cha ishirini na mbili (22) cha baraza la Wafanyakazi la MSD Mkoani Morogoro ambapo amesisitiza kuwa, kujali wateja ni msingi wa kuwahudumia kulingana na mahitaji yao.