Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi MSD, Watembelea Mbuga ya Taifa ya Tarangire
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Bohari ya Dawa (MSD) wametembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire lengo likiwa ni kujionea vivutio mbalimbali vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ambayo inapatikana ndani ya mkoa wa Manyara.
Ziara hiyo imekuja ili kuongeza chachu na kuhamasisha wageni na watumishi mbalimbali kuweza kutembelea vivutio vyetu vya utalii vilivyoko nchini, ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Kutangaza utalii nchini.