Skip to main content
  • Watumishi wa MSD Wajengewa Uwezo, Juu ya Mifumo ya Usimamizi Ubora

    Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wanaosimamia mifumo ya Usimamizi wa Ubora  (QMS) wamejengewa uwezo ili kutekeleza na kusimamia majukumu yao kwa ufanisi na weledi kazinini.

    Akimzungumza wakati wa kufunga Mafunzo hayo, Kaimu Meneja wa Udhibiti Ubora wa MSD, Bi. Estella Meena alisema mafunzo hayo maalum yanatarajiwa kuwa chachu kuhakikisha matakwa ya ithibati ya Ubora wa kimataifa, yaani  ISO 9001:2015 yanatekelezwa kikamilifu, hivyo kuboresha utendaji na kuhakikisha malengo ya taasisi yanafikiwa.

  • MSD na CRDB Wabadilishana Uzoefu

    Katika hatua ya kuongeza ujuzi katika utoaji wa huduma kwa wateja Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wa Kurugenzi ya Ugavi wanaofanya kazi kwenye Idara ya Huduma kwa Wateja wametembelea Ofisi za Makao Makuu ya Benki ya CRDB zilizopo jijini Dar es Salaam. 

    Lengo la ziara hiyo ni kubadilishana uzoefu na kujifunza namna Benki hiyo inavyotoa huduma kwa wateja wake na namna inavyoweza kusimamia na kutatua malalamiko ya wateja. 

  • MSD Yashiriki Shughuli za Kijamii na Kutembelea Wateja Wake, Ikiadhimisha Miaka 30 ya Utendaji Toka Ianzishwe

    Katika maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Wateja kwa mwaka huu 2024, ambayo yalienda sambamba na sambamba na shughuli za kuadhimisha miaka 30 ya MSD, jumla ya wateja 18 walitembelewa kupitia kanda zote za MSD na kujadiliana masuala mbalimbali ya kuboresha Huduma zinazotolewa na MSD pamoja na mahusiano na ushirikiano na wateja.

  • Mganga Mkuu Mkoa wa Pwani, Apongeza Ushirikiano Baina ya MSD na Wateja Wake.

    Bohari ya Dawa(MSD) Kanda ya Dar es Salaam imeandaa kikao kazi na wadau wake wa mkoa wa Pwani kilichofanyika Mkoani Pwani - Wilayani Kabaha katika Chuo cha Mwalimu Nyerere  kuzungumza kwa pamoja namna ya koboresha upatikanaji wa bidhaa za afya.

    Akizungumza kwenye kikao hicho Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Dkt. Urio Kusirye amesema vikao kazi hivyo ni muhimu kwani vinachangia kuhakikisha huduma za afya ndani ya Mkoa wa Pwani zinakuwa endelevu na bora.

  • Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi MSD, Watembelea Mbuga ya Taifa ya Tarangire

    Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Bohari ya Dawa (MSD) wametembelea Hifadhi ya Taifa ya Tarangire lengo likiwa ni kujionea vivutio mbalimbali vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ambayo inapatikana ndani ya mkoa wa Manyara.

    Ziara hiyo imekuja ili kuongeza chachu na kuhamasisha wageni na watumishi mbalimbali kuweza kutembelea vivutio vyetu vya utalii vilivyoko nchini, ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Kutangaza utalii nchini.

About

MSD ilianzishwa kwa madhumuni ya uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya zilizoidhinishwa zinazohitajika kutumiwa na vituo vya afya. Katika kutekeleza dhamira hii, tunahakikisha kuwa bidhaa za afya nchini Tanzania zinapatikana, zinategemewa, na zinauzwa kwa bei nafuu lakini pia zinatolewa kwa wakati katika vituo vyote vya afya nchini Tanzania na kwingineko.

Featured Posts

Contact info

Dhamira yetu: Kufanya bidhaa bora za afya kufikiwa na vituo vyote vya afya vya umma nchini Tanzania.