Mkuu wa Mkoa wa Njombe Atembelea Kiwanda cha MSD-Idofi
NJOMBE
Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Antony Mtaka na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Njombe imetembelea kiwanda cha Bohari ya Dawa (MSD) cha kuzalisha mipira ya mikono kilichopo Idofi, Makambako ambacho ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 70.
Mhe.Mtaka amesema kiwanda hicho ni muhimu kwa sekta ya afya kwani kitapunguza matumizi ya fedha za kigeni kununua bidhaa hiyo nje ya nchi na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa mipira ya mikono nchini.