Skip to main content

Wadau na wateja wa MSD wamekumbushwa kuendelea kushirikiana

Wadau na wateja wa MSD wamekumbushwa kuendelea kushirikiana kwa karibu ili kihakikisha wanaendelea kuboresha upatikanaji wa bidhaa  za afya nchini na kuwa utaratibu wa kulipa madeni ili kuiwezesha MSD kuwa na mtaji mzuri wa kuendelea kununua bidhaa za afya.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt.Charles Rashid Mkombachepa alipokuwa anafungua kikao cha mwaka cha wadau na wateja wa MSD kanda ya Kilimanjaro wa mkoani wa Arusha. Dkt. Mkombachepa amewakumbusha watendaji hao kuwa ubora wa huduma za MSD tunazoziona leo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya umechangiwa na upatikanaji mzuri wa fedha za kuiendesha MSD.

Hata hivyo Dkt. Mkombachepa ameipongeza MSD kwa kuboresha huduma kwa mkoa wa Arusha ambapo huduma hizo zilizoboreshwa zimewezesha kuongezeka kwa upatikanaji wa bidhaa za afya hadi kufikia zaidi ya asilimia 90%.

Dkt.Mkombachepa amesema kutokana na maboresho hayo ambayo MSD inayafanya, malalamiko yamepungua, lakini amesisitiza kuwa ni vizuri tukakaa pamoja na kutatua changamoto chache zilizobakia ili  kuzungumzia maboresho zaidi kuliko malalamiko.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha wa MSD Undule  Koroso amesema vikao hivi vina umuhimu kwa MSD kwani vinaboresha mahusiano na mawasiliano kati ya MSD na wataja wake na wateja wanapata wasaa wa kukutana ana kwa ana na MSD kuzungumza masuala ya kuboresha katika mnyororo mzima wa bidhaa za afya.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.