MSD Yakabidhi Vifaa Tiba vya Mil. 114 - Kituo cha Afya Mtae
SERIKALI imetoa Sh.Milioni 114 kwa Kituo cha Afya Mtae kilichopo Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga ambazo zimetumika kununulia vifaa tiba kupitia Bohari ya Dawa (MSD) na hivyo kinatarajia kuanza kutoa huduma ya upasuaji mwishoni mwa mwezi Disemba 2023.