MSD Yapongezwa kwa Mageuzi ya Huduma, ndani ya Muda Mfupi.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makorora mkoani Tanga, Dkt.Angelina Meshack ameipongeza serikali kupitia MSD, baada ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji ikiwemo kitanda cha upasuaji, mashine ya dawa ya usingizi na taa zinazotumika wakati wa upasuaji, amesema vifaa hivyo ni msaada mkubwa katika kituo hicho kwani awali kulikuwa na changamoto kwenye hutoaji huduma.