Mhe. Queen Sendiga Aipongeza MSD.
Rukwa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Sendiga amefurahishwa na huduma za MSD Mkoani humo na kusema kwamba hivi sasa huduma za afya hasa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarika kwa kiasi kikubwa.
Mhe. Sendiga ameongeza kuwa huduma na uhusiano wa MSD na Uongozi wa Mkoa wa Rukwa umeimarika na kwamba kero mbalimbali zilizokuwepo hapo awali, mathalani za upungufu wa bidhaa za afya sasa zimetatuliwa kwa kiasi kikubwa.