MSD YATUNUKIWA TUZO YA UMAHIRI WA UTOAJI HUDUMA
Bohari ya Dawa (MSD), imetunukiwa tuzo ya umahiri wa utoaji huduma kwenye sekta ya Famasi nchini (Award of Service Excellence in Pharmaceutical Sector) kupitia tuzo za mwaka za Tanzania Service Excellence Award 2024, zilizoandaliwa na taasisi ya Charted Institute of Customer Service (CICM) Tunzo hizo zimetolewa hapo jana na taasisi hiyo katika hafla maalum iliyofanyika katika ukumbi wa Holiday In, jijini Dar es Salaam