MSD YATUNUKIWA TUZO KWA KUWEZESHA MATIBABU YA MOYO NCHINI
Bohari ya Dawa (MSD) imetunukiwa tuzo maalum na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kutambua mchango na ushirikiano wake katika kuboresha huduma na matibabu ya Programu za Moyo nchini.
Tuzo hiyo maalum, imekabidhiwa na Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Nassor Ahmed Mazrui, wakati akifunga mkutano wa siku tatu wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo, ulioandaliwa na taasisi hiyo ya JKCI, na kukutanisha Wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi, madaktari, watafiti, wasambazaji Dawa na Vifaa tibawa visiwani humo.