Rais Samia Apeleka Tabasamu Kwa Wananchi wa Kata ya Magazini - Wilaya ya Namtumbo
Kituo cha Afya cha Magazini kilichopo Kata ya Magazini Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma kimepata msaada wa vifaa Tiba vya kisasa vya upasuaji vikiwemo vya wamama wajawazito vyenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 100 ili kuweza kusaidia kuboresha huduma za afya kwenye kata hiyo, iliyoko mpakani na nchi ya msumbiji .