Waziri Jenista Mhagama Apongeza Mradi wa Ujenzi wa Ghala la Kisasa la MSD-Dodoma
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama February 6, 2025 ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma, na kupongeza hatua za maendeleo ya mradi huo wa kimkakati ambao umefikia. asilimia 85%.