Serikali Yakabidhi Vifaa Tiba vya Milioni 900 Halmashauri ya Ifakara
#MOROGORO
SERIKALI kupitia Bohari ya Dawa (MSD), imekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya sh milioni 900 kwa Halmashauri ya Ifakara mji.
Akizungumza jana Mkoani humo, Mbunge wa Kilombero Mhe.Abubakar Asenga, alisema ujio wa vifaa hivyo, utasaidia kuboresha huduma za afya hivyo wanaishukuru serikali kwa hatua kubwa ya maboresho katika sekta hiyo.