Mkuu wa Wilaya ya Igunga Apongeza Maboresho ya Huduma za MSD
Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe. Sauda Salum Mtondoo ameipongeza Bohari ya Dawa MSD kwa maboresho ya huduma zake, hali ilipelekea upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za afya nchini, hivyo kuleta unafuu wa huduma kwa watoa huduma na wananchi kwa ujumla wilayani humo.