Aller au contenu principal
  • Mkuu wa Wilaya ya Igunga Apongeza Maboresho ya Huduma za MSD

    Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe. Sauda Salum Mtondoo ameipongeza Bohari ya Dawa MSD kwa maboresho ya huduma zake, hali ilipelekea upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za afya nchini, hivyo kuleta unafuu wa huduma kwa watoa huduma na wananchi kwa ujumla wilayani humo.

  • Ujumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Watembelea Kanda ya Kilimanjaro

    Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini MSD Dkt. Ritah Mutagonda, ambaye pia ni mlezi wa MSD Kanda ya Kilimanjaro ameipongeza Kanda ya MSD Kilimanjaro kwa kuvuka lengo la mauzo kwa kufikia 115% katika kipindi cha nusu mwaka wa fedha 2024/2025.

    Mjumbe huyo wa Bodi ya Wadhamini ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake kwa wateja wanaohudumiwa na Kanda ya Kilimanjaro, kama moja ya shughuli za kuadhimisha miaka 30 ya utendaji wa MSD.

  • Wateja wa MSD Kanda ya Tanga Wapongeza Maboresho ya Huduma za MSD

    Wateja wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Tanga wameipongeza MSD kwa maboresho makubwa inayoendelea kuyafanya ya usambazaji wa bidhaa za afya kwa wakati.

    Pongezi hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD ambaye pia ni Mlezi wa MSD  kanda hiyo, Dkt. Rukia Mwifunyi anayoifanya mkoani humo, kuzungumza na wateja wanaowahudumia ili kupata maoni yao juu ya huduma za MSD na kupokea changamoto zao ili ziweze kufanyiwa kazi.

  • Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Aipongeza Kanda ya MSD Tanga kwa Kuvuka Malengo ya Mauzo

    Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) Dkt. Rukia Mwifunyi amepongeza Kanda ya MSD Tanga kwa kuvuka malengo ya mauzo, katika robo mwaka ya kwanza ya mwaka kwa asilimia 12.

    Mjumbe huyo wa Bodi, ambaye ni mlezi wa Kanda ya MSD TANGA amefuatana na  Meneja Huduma za Sheria MSD, Elisamehe Macha katika ziara ya kutembelea wateja wanaohudumiwa na Kanda ya Tanga,ziara ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka thelathini (30) ya utendaji wa MSD tangu kuundwa kwake.

  • MSD Yapongezwa kwa Mabadiliko na Maboresho ya Kiutendaji Katika Kipindi cha Miaka 30

    Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Dkt. Elisha Robert Ndaki ameipongeza Bohari ya Dawa(MSD) kwa kuboresha huduma kwa wateja, sambamba na upatikanaji wa bidhaa za afya kwa wakati, hali iliyowezesha kupungua kwa malalaiko ya wateja na wananchi kwa ujumla.

    Dkt. Ndaki ametoa pongezi hizo hii leo tarehe 21/11/2024 mbele ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Bw. Ally Seleman wakati ujumbe kutoka MSD ulipotembelea kituo cha Afya Kambarage kilichopo Manispaa ya Shinyanga.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.