UNFPA Yatoa Msaada wa Dawa za Uzazi wa Mpango kwa Serikali ya Tanzania
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshugulikia Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu UNFPA limeikabidhi Serikali ya Tanzania msaada wa dawa za uzazi wa mpango.
Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika Bohari ya Dawa (MSD) Mwakilishi wa UNFPA nchini Tanzania Bw. Mark Bryan Schreiner amesema msaada huo ni sehemu ya jitihada za UNFPA kuisaidia Serikali ya Tanzania kuboresha huduma za uzazi wa mpango kwa wananchi.