MSD Yazindua Kampeni ya Usambazaji Vyandarua Ngazi ya Kaya - Mkoa wa Tabora
MKOA wa Tabora umetajwa kuwa wa kwanza kitaifa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya ugonjwa wa malaria hali inayotokana na imani potofu ya matumizi ya vyandarua vyenye dawa kuwa vinapunguza nguvu za kiume.
Takwimu zinaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa malaria kimeongezeka kutoka asilimia 11.7 mwaka 2016/2017 hadi asilimia 23.4 mwaka 2022 wakati kiwango cha maambukidhi ya malaria kitaifa ni asilimia 8.1.