Skip to main content
  • Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Atoa Rai - Matumizi ya Vyandarua

    Kongwa.

    Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius M. Emmanuel amewataka wakazi na wazazi wote wilayani humo kutumia vyema na kwa lengo lililokusudiwa vyandarua vya msaada wanavyopatiwa serikali, ili adhima ya serikali ya kupambana na ugonjwa wa Malaria iweze kutimia.

    Mhe. Remidius ametoa rai hiyo hii leo wakati akizindua rasmi zoezi la usambazaji wa vyandarua mashuleni wilayani humo, linalofanya na Bohari ya Dawa (MSD).

  • Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Atoa Rai - Matumizi ya Vyandarua

    Kongwa.

    Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius M. Emmanuel amewataka wakazi na wazazi wote wilayani humo kutumia vyema na kwa lengo lililokusudiwa vyandarua vya msaada wanavyopatiwa serikali, ili adhima ya serikali ya kupambana na ugonjwa wa Malaria iweze kutimia.

    Mhe. Remidius ametoa rai hiyo hii leo wakati akizindua rasmi zoezi la usambazaji wa vyandarua mashuleni wilayani humo, linalofanya na Bohari ya Dawa (MSD).

  • Waelimisha Rika MSD Wanolewa

    Dar es salaam

    Waelimisha rika (Pear Educators) ambao ni Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wanapatiwa mafunzo ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UKIMWI pamoja na magonjwa yasiyoambukiza. 

    Mafunzo hayo ya siku tatu yanahusisha waelimika rika kutoka Kanda na Idara zote za MSD, ambao watakuwa waelimishaji watumishi wengine.

  • Watumishi wapya MSD Wapatiwa Mafunzo ya Mifumo

    Watumishi wapya MSD wamepatiwa mafunzo ya namna ya kutumia mifumo ya kiutendaji ya MSD ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao.

    Mafunzo hayo yanayofanyika MSD Keko jijini Dar es Salaam ni ya siku kumi na yanahusisha mifumo yote ambayo watumishi hao wataitumia katika kutoa huduma kwa wateja na wadau mbalimbali wa MSD. 

  • Madereva wa MSD Wajengewa Uwezo

    MOROGORO.

    Watumishi wa MSD wa kada ya Udereva, wameendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo mbalimbali, yanayoandaliwa na taasisi mathalani udereva wa kujihami, alama za barabarani, ukaguzi wa magari, sheria za usalama barabarani, upakiaji wa mizigo na namna bora ya kuendesha magari makubwa yanayovuta tella (truck and trailers) ili kuongeza tija katika kazi zao na taasisi kwa ujumla.

    Mafunzo hayo ya siku 10 yamehusisha nadharia na vitendo na yametolewa na wataalamu kutoka Chuo cha Ufundi Veta, kilichoko Mkoani Morogoro.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.