MSD Yatoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Vifaa Tiba na Maabara Nchini.
Mafunzo ya siku tatu kwa wahandisi vifaa tiba na wataalam wa Maabara nchini, yamefungwa leo mkoani Morogoro.
Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa wakati mmoja kwa mikoa mitano kwa ajili ya wataalam wa nchi nzima yalikuwa na lengo la kuwafundisha wataalamu wa usimikaji, matumizi na ukarabati wa mashine za maabara na vifaa vinavyosambazwa na MSD.