Skip to main content
  • Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Aipongeza MSD kwa Maboresho ya Huduma

    Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameupongeza uongozi wa Bohari ya Dawa (MSD) kwa mabadiliko makubwa yanayoendelea katika taasisi hiyo, ambayo kwa kiasi kikubwa yamewezesha kupunguza malalamiko ya uhaba wa bidhaa za afya nchini, mathalani malalamiko ya uhaba wa dawa.

    Mhe. Senyamule ameeleza kwamba awali wakienda kwenye mikutano ya hadhara kuongea na wananchi, walikumbana na malalamiko mengi ya uhaba wa dawa, lakini hivi karibuni hali imebadilika, japokuwa bado kuna changamoto, lakini angalau inatia moyo kuona kuna mageuzi yanafanyika.

  • MSD KUSAMBAZA VIDONGE MIL. 22 VYA VITAMINI A NCHINI

    Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameikabidhi Serikali ya Tanzania kupitia kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel kwa niaba ya Waziri ya Afya Mhe. Ummy Mwalimu vidonge milion 22  vya matone vya Vitamini A kwa ajili ya watoto, vilivyotolewa na serikali ya Canada, kupitia shirika la Nutrition International (NI). 

    Dkt. Kikwete, amekabidhi dawa hizo akiwa mmoja wa wajumbe wa bodi wa Shirika la kimataifa la Nutrition international ambalo ndio limetoa msaada huo. 

  • MSD Yakutana na Wataalamu wa Maabara Nchini.

    Bohari ya Dawa (MSD), imekutana na wataalam wa maabara ambao ni Mameneja wa maabara za hospitali za Rufaa za Mikoa,Maalum,Kanda na Taifa. Kikao hiki kinachofanyika kwa siku tatu mkoani Dar es Salaam lengo lake ni kutathimini upatikanaji na ubora wa bidhaa za afya za maabara zinazosambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini. 

    Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, amewaeleza washiriki kuwa watumie siku hizi tatu zilizopangwa kuhakikisha wanakuja na majawabu ya changamoto zinazojitokeza katika sekta hii ya maabara. 

  • Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na UKIMWI Yaridhishwa na Utendaji wa MSD.

    Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI imesema  imeridhishwa na hali ya utendaji wa Bohari ya Dawa(MSD) na mipango ya utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo uzalishaji wa dawa ili kupunguza kununua dawa nje ya nchi. 

    Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI, Mhe. Stansilaus Nyongo baada ya kupokea taarifa ya hali ya utendaji na majukumu ya Bohari ya Dawa (MSD), ambapo ameichagiza MSD kuongeza ufanisi, ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha bidhaa za afya zinakuwa toshelevu na  kusambazwa.

  • MSD Yaanza Usambazaji wa Vifaa Tiba kwa Majimbo ya Mkoa wa Morogoro

    BOHARI ya Dawa (MSD) imeanza usambazaji majimboni vifaa  tiba  vilivyonunuliwa na serikali vyenye  thamani ya zaidi ya Sh bilioni 14.9 kwa ajili ya hospitali, vituo vya afya na zahanati  lengo ni kupunguza vifo vya mama na mtoto.

    Meneja wa MSD, Kanda ya Dar es salaam, inayohudumia mikoa ya  Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Visiwa vya Zanzibar, Betia Kaema alisema hayo wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Adam Malima kwa ajili ya majimbo 11 ya Mkoa huo.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.