Skip to main content
Waelimisha Rika wa MSD, Wakipokea Mafunzo Kutoka kwa Mkufunzi Kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Waelimisha Rika MSD Wanolewa

Dar es salaam

Waelimisha rika (Pear Educators) ambao ni Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) wanapatiwa mafunzo ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UKIMWI pamoja na magonjwa yasiyoambukiza. 

Mafunzo hayo ya siku tatu yanahusisha waelimika rika kutoka Kanda na Idara zote za MSD, ambao watakuwa waelimishaji watumishi wengine.

Sera ya MSD ya kukinga watumishi dhidi ya UKIMWI na magonjwa yasiyoaambukiza inaeleza kuwa kila Kanda na Idara ya MSD inatakiwa kuwa na mueleimisha rika ili aweze kuwasaidia watumishi wengine namna ya kujikinga dhidi ya UKIMWI na magonjwa yasiyoambukiza. 

Mkufunzi kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Kweka amesema Elimu ya UKIMWI mahali pa kazi inawawezesha watumishi kuzingatia mihimili muhimu kuwa na uhakika wa elimu na habari za magonjwa tajwa, mafunzo,ufahamu wa kupima kwa hiari, matunzo na kusaidia waathirika.

Aidha watumishi watakuwa chachu katika kampeni ya kujikinga na kudhibiti magonjwa hayo.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.