MSD Yakutana na Wataalamu wa Maabara Nchini.
Bohari ya Dawa (MSD), imekutana na wataalam wa maabara ambao ni Mameneja wa maabara za hospitali za Rufaa za Mikoa,Maalum,Kanda na Taifa. Kikao hiki kinachofanyika kwa siku tatu mkoani Dar es Salaam lengo lake ni kutathimini upatikanaji na ubora wa bidhaa za afya za maabara zinazosambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, amewaeleza washiriki kuwa watumie siku hizi tatu zilizopangwa kuhakikisha wanakuja na majawabu ya changamoto zinazojitokeza katika sekta hii ya maabara.