MSD Kuja na Suluhu ya Special Procurement
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, ambaye pia ni mlezi wa Kanda ya MSD Kagera Bi. Rosemary Slaa, amewahakikishia wataalamu wa afya kutoka Mikoa ya Kagera na Geita kuwa Bohari ya Dawa (MSD) inaendelea kufanya maboresho katika upatikanaji wa bidhaa za afya nchini, mathalani upatikanaji wa vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa wakati.