Skip to main content
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande ( wapili kulia), Akiwa Kwenye Picha ya Pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe (wa kwanza kushoto), pamoja na Viongozi Wengine Kutoka MSD na Benki ya TDB Wakati wa Makabidhiano ya Msaada wa Vifaa vya Kujikinga dhidi ya UVIKO 19, Uliotolewa na Benki ya TDB.

Tanzania Yapokea Msaada Kutoka Benki ya TDB

DAR ES SALAAM: 

Serikali ya Tanzania, imepokea msaada wa shilingi milioni 230 kutoka Benki ya Biashara na Maendeleo (TDB) kwa ajili ya kununulia vifaa vya kujikinga na kupambana na ugonjwa wa Uviko-19.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Uongozi wa benki hiyo, Mkurugenzi wa Uhusiano na Uwekezaji Bi. Mary Kamari, amesema benki yake imetoa msaada huo ili kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika miradi mbalimbali kimkakati ili kuwaletea Watanzania maendeleo.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya serikali, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), ameipongeza benki hiyo kwa mchango wake kwa sekta ya afya, huku akiisihi kuendelea kushirikiana na serikali kwenye nyanja mbalimbali za maendeleo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe amesema Wizara imepokea msaada huo kwa unyenyekevu mkubwa kwani utasaidia katika mapambano ya milipuko ya magonjwa yanayoshabihiana na Uviko-19 mathalani mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, uliozikumba nchi jirani.

 

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.