Skip to main content

MSD KUSAMBAZA VIDONGE MIL. 22 VYA VITAMINI A NCHINI

Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameikabidhi Serikali ya Tanzania kupitia kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel kwa niaba ya Waziri ya Afya Mhe. Ummy Mwalimu vidonge milion 22  vya matone vya Vitamini A kwa ajili ya watoto, vilivyotolewa na serikali ya Canada, kupitia shirika la Nutrition International (NI). 

Dkt. Kikwete, amekabidhi dawa hizo akiwa mmoja wa wajumbe wa bodi wa Shirika la kimataifa la Nutrition international ambalo ndio limetoa msaada huo. 

Akikabidhi dawa hizo ameeleza kuwa lengo ni  kuwasaidia watoto na dawa hizo zitatolewa kwa awamu mbili  yaani mwezi Juni na Disemba kwa watoto takribani milioni 11 walio chini ya umri wa miaka mitano.

Dkt. Kikwete ameeleza kuwa vitamini A husaidia kuimarisha afya ya macho  na kuongeza kinga ya mwili kwa mtoto hivyo ni muhimu kwa wazazi kuhakikisha watoto wanapatiwa matone haya.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema Serikali kupitia Wizara afya inashukuru na  imepokea vidonge vya matone ya Vitamini A milioni 22 kutoka kwa shirika la Nutritrion International, ambayo itasaidia watoto milioni 11.

Aneongeza kuwa elimu ya mtoto inaanza tangu siku  mimba inatungwa, kwa kumpatia Mama lishe bora wakati wa ujauzito ili kusaidia kuimarisha ubongo wa mtoto, hivyo amewakumbusha wazazi kuzingatia lishe bora kwa watoto tangu wa utangaji wa mimba na kuwa na desturi ya kula mlo bora kwa mama wajawazito.

Dawa hizo zimehifadhiwa Bohari ya Dawa (MSD) na zitasambazwa kwa kuzingatia mgawo utakaotolewa na Wizara ya Afya katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

MSD imekuwa msambazaji mkuu wa dawa hizo na nyingine kadha wa kadha kwa kuhakikisha dawa hizo zinawafikia wananchi kupitia vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya nchini, zahanati na hospitali.

About MSD

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by all public health facilities.