Wananchi Wilayani Chemba Waipongeza Serikali kwa Kuboresha Huduma za Afya

 

MSD_DRIVER.jpgMSD_CSO.jpg_MG_9426.jpg_MG_9435.jpgMWENYEKITI.jpg_MG_9431.jpg

Wananchi wa Kata ya Sanzawa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma wameipongeza Serikali kwa kuboresha huduma za afya kuwapelekea dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa wakati jambo ambalo limewaondolea usumbufu wa kupata matibabu wanapoumwa.

Pongezi hizo walizitoa kwa nyakati tofauti wilayani humo wakati wakizungumza na waandishi wa habari pamoja na maofisa wa Bohari ya Dawa (MSD), ambao wanawatembelea wateja wao katika vijiji vya Mkutimango na Minyembe kujua changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Mkazi wa Kijiji cha Moto, Ali Tengeneza alisema anaipongeza MSD na Serikali kwa kufanikisha kuwafikishia dawa kwa wakati tofauti na miaka ya nyuma ambapo walikuwa wakilazimika kwenda kuzinunua katika maduka ya watu binafsi.

" Watu katika familia yangu wakiumwa huwa nawaleta kutibiwa katika Zahanati yetu hii ya Kijiji cha Sanzawa na hakuna siku waliyokosa dawa " alisema Tengeneza.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Sanzawa, Shabani Msemule alisema hapo awali walikuwa na changamto ya upatikaji wa dawa lakini hivi sasa haipo na dawa zinapo kuwa zimekwisha katika zahanati hiyo huwa wanakwenda kutibiwa Kituo cha afya cha Kwamtolo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uendeshaji wa zahanati hiyo, Iddi Degera alisema hivi sasa hakuna changamoto ya upatikanaji wa dawa kwenye zahanati hiyo dawa na mahitaji mengine yanayohusu afya yanapatikana.

Mkazi mwingine wa Kata hiyo, Nicholaus Dominick aliiomba serikali kuboresha zaidi miundombinu ya zahanati na vituo vya afya.

Mjumbe wa Kamati ya Afya ya Kijiji hicho, Flaviana Joseph alisema mara kwa mara wamekuwa wakipokea dawa kutoka MSD na kuzipokea kwa utaratibu uliopo na orodha ya dawa zote wanazozipokea na thamani yake hubandikwa kwenye ubao wa zahanati hiyo ili kila mwananchi aweze kuona.

Muuguzi Msaidizi na Mkunga wa zahanati hiyo, Dativa Kiabuka alisema dawa zote muhimu wamekuwa wakizipata kwa wakati na hawajawahi kupungukiwa kutokana na utaratibu waliojiwekea wa kutoa oda pale wanapoona zinapungua na kuwa katika eneo hilo magonjwa yanayosumbua zaidi ni malaria,kukooa na matumbo na kuwa wagonjwa wanaotibiwa ni kuanzia 20 hadi 50 kwa siku.


 

Waziri Ummy Aipongeza MSD Kununua Dawa SADC

 

UMMY_SADC.jpg4.jpg

                   Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

              Mhe.Ummy Mwalimu (Mb) amesema hatua ya MSD kununua dawa

             za SADC itasaidia kupunguza gharama za kununua dawa kwa nchi

                            husika na kuboresha upatikanaji wa dawa.

 

                Ameeleza kuwa kwa nchi moja moja kununua dawa ni gharama,

              ndio maana serikali ya Tanzania kupitia MSD imeteuliwa kufanya

           manunuzi ya pamoja ya dawa kwa nchi hizo,na tayari wameshatangaza

                                                     zabuni.

 

                  Waziri huyo ameeleza hayo kwa waandishi alipotembelea banda

                     la MSD kwenye Maonesho ya wiki ya viwanda yanayoendelea

               jijini Dar es Salaam yanayoshirikisha wadau kutoka nchi mbalimbali

                                                    za Afrika.

 

               Maonesho ya viwanda ni utangulizi wa mkutano wa 39 wa SADC 2019,

                       ambao mwaka huu Tanzania ni mwenyeji wa mkutano huo .

 

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Yaipongeza MSD kwa Kupata Hati Safi ya Ukaguzi wa Hesabu Zake

EA183DD7-8E1F-4CCF-8505-4ECE49AC4CCC.jpeg

Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe.Naghenjwa Kaboyoka ameipongeza MSD kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu zake, na kuitaka kuendeleza rekodi hiyo safi kwa ustawi wa taasisi hiyo kiutendaji.

Ametoa pongezi hizo leo Kamati hiyo ilipokuwa ziarani MSD, ambapo ilipokea taarifa ya utendaji ambayo inafafanua mikakati ya maboresho ya utendaji wa MSD, mwenendo wa mapato na matumizi ya fedha na Mnyororo wa Ugavi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara.

Ameipongeza pia MSD kwa kuteuliwa kuwa mnunuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na kusema kuwa hiyo ni heshima kubwa kwa Taifa.

287978CA-DC65-4294-A262-D3E7E858A3CB.jpeg

Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Dkt. Fatma Mrisho ameihakikishia Kamati hiyo kuwa, pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili MSD bado inaendelea kutoa huduma bora na za kiwango cha juu kwa wananchi na kusimamia mnyororo wa ugavi ili kuleta tija kwenye mfumo wa afya wa nchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean R. Bwanakunu amesema MSD inajipanga sasa kuhakikisha inafanyia kazi maoni na

maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na kamati hiyo kwani ni maelekezo yenye lengo la kuiboresha MSD, ili izidi kutimiza majukumu yake ya kila siku

kwa ufanisi katika kuwahudumia wananchi.

87AA4840-2F96-472A-8DE6-5DC7D148B3F7.jpeg

CANCELLATION OF MSD PUBLIC AUCTION

CANCELLATION OF MSD PUBLIC AUCTION 

TO DISPOSE MSD UNSERVICEABLE FIXED ASSETS BY PUBLIC AUCTION

This is to inform the General Public that the Public Auction Advert which appeared in the local newspapers on 2nd, 7thand 14thMay, 2019 on Daily News, Uhuru and Jamhuri respectively has been cancelled due to the unavoidable circumstances until further notice.

Any inconvenience is highly regretted.

THE DIRECTOR GENERAL

Medical Stores Department,

Off Nyerere Road, Keko Mwanga

P.O. Box 9081

Dar-es Salaam

                                        

Tel: 255 22 2860890-7

Fax: No. 255 22 28658114/19

Email:This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Website:www.msd.go.tz

MSD na SADC Wajadili Muongozo wa Manunuzi ya Pamoja ya Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi

 

 

 

 

626963FD-CE3A-41E5-B318-3000BD2C6C78.jpeg

Bohari ya Dawa (MSD) kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imeratibu Mkutano wa wataalamu wa manunuzi ya pamoja (SADC Pooled Procurement Services (SPPS) unaofanyika jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ilikuwa ni kupitia mwongozo wa manunuzi wa pamoja wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi wanachama wa SADC. 

Akifungua mkutano huo, Mfamasia Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Bw. Daudi Msasi amewashukuru wawakilishi wa nchi wanachama wa SADC kwa kuitikia wito wa kushiriki kwenye mkutano huo na kwa kuiamini Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa za pamoja. 

Aidha Bw. Msasi pia ameeleza kuwa MSD imekuwa miongoni mwa taasisi bora barani Afrika zinazo shughulika na mnyororo wa ugavi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara. 


3CDE457D-B3FD-4B16-A9ED-2E12224BDA1C.jpeg

 

 

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Manunuzi wa MSD Bw. Abdul Mwanja amesema MSD imejipanga kuanza utekelezaji wa jukumu hilo na tayari imeshatekeleza jukumu hilo kama lilivyoainishwa katika Hati ya Makubaliano na Sekretariati ya SADC (MoU) kwa kuanzisha kitengo kitakachoshughulikia manunuzi hayo kwa upande wa SADC. 

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema, faida ambazo nchi wanachama wa SADC watazipata ni pamoja na kupata dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa bei nafuu na vyenye ubora, kuboresha kiwango cha usambazaji kwa kila nchi mwanachama. 


CAB58CBD-363C-4E50-B6D1-BFE8B3E18AA6.jpeg

 

Ameongeza kuwa kupatikana kwa fursa hii ni heshima kubwa kwa Tanzania, hatua ambayo italeta ushirikiano ndani ya kanda na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, pia kuongeza fursa uwekezaji wa viwanda vya kuzalisha dawa na vifaa tiba kwa nchi za SADC na nje, hivyo kupanua soko.

 

Tanzania kupitia MSD ilishinda zabuni ya kuwa mnunua wa pamoja wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa niaba ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

 

1DF4DD23-E561-4819-A056-047319435CC2.jpeg

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker