Mawaziri wa Afya wa SADC Waitembelea MSD

4.jpg

                                 (Mawaziri wa Afya kutoka nchi za SADC wakimakinikia mada, mara walipotembelea MSD)

               Mawaziri kutoka Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Africa

                (SADC) wanaoshughulikia masuala ya Afya na Ukimwi

           wametembelea Ofisi za Bohari ya Dawa (MSD) zilizoko Keko,

                  jijini Dar es Salaam nakushuhudia jinsi mnyororo

                            mzima wa ugavi unavyofanya kazi.

 

                 Mawaziri hao wameonyesha kuridhishwa na kufurahishwa

                   na jinsi MSD ilivyojipanga katika kutekeleza majukumu

               yake kwa ufanisi,mathalani ununuzi, uhifadhi, na usambazaji

                     wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara huku

              wakibainishakuwa ni mfano wa kuigwa kwa nchi wanachama.

3.jpg

                     (Mawaziri wa Afya kutoka nchi za SADC wakimakinikia mada,

                                mara walipotembelea Bohari ya Dawa (MSD))

        Mawaziri hao wanaoshughulika na afya wameambatana na mwenyeji

             wao Waziri wa afya wa Tanzania, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb),

               ambaye amewaeleza waandishi wa habari utayari wa MSD

                 katika katika kufanya manunuzi ya pamoja kwa nchi

              za SADC na mchakato mzima uliopelekea MSD kupewa

                                              zabuni hiyo.

 

 

                 Aidha, amebainisha kuwa lengo la ziara hiyo ya Mawaziri

                 ni kuangalia uwezo, vifaa na utaalamu wa MSD katika

                     kutekeleza majukumu hayo kwa nchi wanachama.

 

index2.jpg

                           (Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean Bwanakunu, akitoa mada)

               Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean             

             Bwanakunu, ametoa tathimini ya ulipofikia mchakato mzima

          wa manunuzi ya pamoja, kwa nchi wanachama hadi sasa (SPPS),

             ambapo amebainisha kwamba wamekwisha pata wazabuni

                     na sasa mikataba iko kwa Mwanasheria Mkuu

                                 ikifanyiwa upembuzi, (Vetting).

 

 

               Aidha amewahakikishia mawaziri hao kutoka SADC kuwa

        mchakato wa manunuzi ya pamoja utapunguza gharama kwa kiasi

      kikubwa kwa nchi wanachama na kukuza uchumi wa viwanda kupitia

                                     uwekezaji wa viwanda vya dawa.

 

 

               Mawaziri hao kutoka SADC, walipata fursa ya kutembelea

              magahala ya kuhifadhia dawa ya MSD na kujionea jinsi kazi

               mbalimbali za utunzaji na ugavi, zinavyofanyika kwa weledi

                                         na ufanisi mkubwa.

 

index.jpg

(Meneja Mradi Msonge wa MSD Bw. Bill Singano, akitoa ufafanuzi mbele ya mawaziri wa Afya wa SADC)
 

DKT. Shein Amwaga Pongezi kwa MSD.

DKT_SHEIN.jpg3.jpg

                          Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi

                    Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein ameipongeza MSD kwa kuteuliwa

                           kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa ajili ya nchi za SADC.

 

                                Dkt. Shein alimweleza hayo Mkurugenzi Mkuu wa MSD

                        Laurean Bwanakunu alipotembelea banda la MSD katika maonesho

                                  ya viwanda yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

 

                  Kingozi huyo pia ameishauri MSD kuwatembelea wazalishaji wakubwa

                       wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara wa mataifa

                     ili wapate taarifa sahihi na kuwashirikisha kuhusu MSD kuteuliwa

                        kusimamia manunuzi ya pamoja ya dawa kwa nchi za SADC.

 

                           DKT_SHEIN.jpg                               

                          

                     Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu

                   amesema tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya manunuzi ya pamoja,

                   ambapo tayari wameanza mchakato wa kupata wazabuni na kuanzisha

                mfumo wa kielektroniki utakaotumiwa na nchi wanachama kuleta mahitaji.

 

               Bohari ya Dawa MSD, ni moja ya taasisi zilizoshiriki maonyesho ya biashara

              na viwanda ya SADC yaliyofanyika wakati wa wiki ya mkutano wa SADC 2019,

                   katika viwanja vya kimataifa vya Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

Waziri Ummy Mwalimu, Ahimiza Ujenzi wa Viwanda vya Dawa Nchini

5555555555.jpg

                                ,

 

        Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu

          amesema serikali inawajengea mazingira mazuri wazalishaji dawa,vifaa tiba na

     vitendanishi vya maabara wanaowekeza nchini kwani wanasaidia kupunguza gharama

                                                za kuagiza dawa nje ya nchi.

 

        Waziri Huyo ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa Tatu wa mwaka

        wa wazalishaji na wasambazaji Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi vya Maabara

                                       kutoka nchi mbalimbali duniani.

 

7777777777.jpg

 

            Mkutano huo umeandaliwa na Bohari ya Dawa kwa kushirikiana na UNDP

             ambapo mwakilishi wa UNDP Dr. Rosemary Kumwenda amesema mkutano

           huu ni muhimu kwani MSD kwa sasa inafanya kazi kimataifa na UNDP kama

             wakala wa maendeleo wa Umoja wa Mataifa inawajibu wa kuunga mkono

           jitiada za MSD kuhakikisha shughuli zinazofanywa na MSD zinakuwa na              

                                                  manufaa kwa wananchi.

 

6666666666666.jpg

 

           Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema wameandaa

               mkutano huo ili kuweka mazingira ya uwazi na kuboresha utendaji wa

         MSD na kuwavutia wazalishaji wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi vya Maabara

                                                        kuja kuwekeza.


 

MSD Yawasilisha Msaada wa Dharura kwa Majeruhi wa Ajali ya Moto Mkoani Morogoro

MOROGORO_CSR.jpg

                                ,

 

      

                                         Timu ya MSD ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD

                                Bw. Laurean Bwanakunu wakiwa sambamba na Mganga Mkuu wa Serikali

                                   Prof. Mohamed Kambi, wamewatembelea majeruhi wa ajali ya moto,

                                iliyosababishwa na mlipuko wa lori la mafuta waliolazwa katika hospitali

                                                             ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

 

                                                                MOROGORO_CSR.jpg4.jpg

 

                                 Pamoja na kuwajulia hali majeruhi hao, ujumbe huo pia ulilenga

                               kufuatilia na kufahamu misaada ya haraka ya kitabibu inayohitajika

                                            kwa sasa hospitalini hapo ili kusaidia majeruhi.

                                                              MOROGORO_CSR.jpg3.jpg

 

                          Aidha, Bohari ya Dawa imechukua jitahada za makusudi kwa kusafirisha

                                shehena hiyo kutoka kwenye magahala yake jijini Dar es salaam,

                                                  ili kuokoa maisha ya watanzania wenzetu.

 

 

 

 


 

Waziri Bashungwa Asema Serikali Imeweka Mazingira Rafiki kwa Uanzishwaji wa Viwanda Nchini

waziri_pp.jpg

                                ,

 

Waziri wa Viwanda na Biashara nchini Mhe. Innocent Bashungwa amefungua mkutano

wa kwanza wa kimataifa wa wawekezaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba,ulioandaliwa

na Bohari ya Dawa (MSD).

 

Waziri huyo ameeleza kuwa kufuatia sera ya Tanzania ya viwanda, serikali

imewekamazingira rafiki ya uwekezaji wa viwanda vya kuzalisha dawa nchini ili

kuwawezesha wawekezaji wenye nia.

 

Amesema hatua hiyo itapunguza pia utegemezi mkubwa wa dawa na vifaa tiba

kutokanje ya nchi, kwani kwa sasa taifa linapoteza fedha nyingi za kigeni katika

kununulia bidhaa hizo za afya.

 

 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema wameandaa mkutano

huo ili kuweka mazingira ya uwazi kupata wawekezaji,ambapo wamewaeleza matokeo

ya utafiti uliofanywa na mshauri mwelekezi wa mradi wa uanzishaji viwanda vya dawa

kwa ubia wa sekta ya umma na sekta binafsi.

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker