Waziri wa Afya Zanzibar Aipongeza MSD

waziri_4.jpg

                   Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mzrui

              Akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze,wakati

               alipotembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa Yaliyoko Keko Jijini Dar es Salaam

 

Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mzrui ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) kwa hatua kubwa iliyochukua katika kuanzisha viwanda nchini, kwani itasaidia katika kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini, sambamba kuboresha afya za wananchi.

 

Mhe. Mazrui ametoa pongezi hizo leo tarehe 20/8/2021 baada ya kutembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa yaliyoko Keko jijini Dar es Salaam, ili kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Bohari hiyo, mathalani mipango yake ya uzalishaji wa dawa na vifaa tiba.

 

“Nimevutiwa na hatua za MSD kuamua kuzalisha bidhaa za afya yenyewe, Mkurugenzi Mkuu na Menejimenti ya MSD nawapongeza sana, Sisi kama Serikali ya Mapinduzi Zanzibar tutaangalia namna tunaweza kushirikiana ili kupanua wigo wa kuboresha huduma za afya. Kiukweli naichukulia MSD kama sehemu ya Wizara ya Afya Zanzibar. “” Alisema Mhe. Mazrui.

 

waziri_2.jpg

                         Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mzrui 

                 Akipokea maelezo kutoka kwa Msimaizi wa Kiwanda cha Barakoa cha MSD Bw. Twahil Magoolo

                                wakati alipotembelea kiwanda hicho kilichoko Keko Jijini Dar es Salaam

 

Katika hatua nyingine Mhe. Mazrui ametembelea viwanda vya MSD ikiwa ni pamoja na Keko Pharmaceuticals na kiwanda cha kuzalisha barakoa na kujionea hatua mbalimbali zilizofikiwa katika uzalishaji, na baadae alitembelea Kanda ya Dar es Salaam huku akipongeza uongozi kwa kazi kubwa zinazofayika na kuwataka kuendelea kujituma ili kuboresha sekta ya afya.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze (Dkt) ameeleza jitihada mbalimbali alizozifanya toka ateuliwe kushika wadhifa huo, kwani zimesaidia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha huduma za afya nchini.

 

waziri_5.jpg

                     Mhe. Nassor Ahmed Mzrui Akipokea maelezo kuhusu dawa kutoka kwa Mtaalamu wa Kiwanda cha

                                MSD- Keko wakati alipotembelea kiwanda hicho kilichoko Keko Jijini Dar es Salaam

 

“Toka nimeteuliwa tumeshirikiana vizuri na Menejimenti yangu kwa pamoja tumejitahidi kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba nchini, ujenzi wa viwanda na mageuzi ya kiutendaji, ninayo Imani kubwa kwamba siku si nyingi, ile adhima ya serikali ya kuboresha afya ya kila mtanzania inaenda kutimizwa kwa kiasi kikubwa kufuatia mageuzi makubwa tunayofanya” Alisema Meja Jenerali Mhidze.

 

Aidha ameongeza kuwa, ifikapo mwezi wa 10 mwaka huu, Kiwanda cha Mipira ya Mikono, na pamoja na viwanda vingine vya dawa, vinavyojengwa Makambako Mkoani Njombe vitaanza kufanya kazi, hivyo kuboresha huduma za upatikanaji wa dawa na vifaa tiba.

 

waziri_7.jpg

                                 Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mzrui

                                Akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze,

                na baadhi ya watumishi  wa MSD wakati alipotembelea Kanda ya MSD-Dar es Salaam (Dar Zone)

 

Ameongeza kuwa, kwa dawa na vifaa tiba ambavyo uchakataji wake ni mgumu, tayari MSD imenza kuingia mikataba ya ubia na wazalishaji wa huduma hizo, lengo likiwa ni kupunguza gharama za upatikanaji wa huduma hizo nchini, na kuleta unafuu kwa mwananchi wa kawaida ambalo ndio lengo hasa la serikali.

 

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE

Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mzrui Akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze,wakati alipotembelea Makao Makuu ya      Bohari ya Dawa Yaliyoko Keko Jijini Dar es Salaam

MSD Yaendesha Mafunzo ya Tehama kwa Watumishi Wake

1111111.jpg

                           Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala MSD Bw. Erick Mapunda,

                                               Akisisitiza Jambo Wakati wa Mafunzo

 

 

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa MSD Bw. Erick Mapunda amewaasa watumishi wa MSD kutotumia vibaya mifumo ya taasisi kwa kufanya matendo yasiyofuata utaratibu na kanuni za utumishi wa umma, bali watumie uzoefu wao kubaini changamoto zote za kimfumo ili ziweze kupatiwa ufumbuzi na kuhakikisha Taasisi inafikia malengo yake.

 

Bw. Mapunda ametoa rai hiyo hii leo tarehe 9/8/2021 jijini Dar es salaam, wakati akifungua mafunzo ya siku 7 yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wa MSD juu ya maboresho ya Mfumo wake wa EPICOR 10, uliohuishwa hivi karibuni ili kuboresha huduma kwa wateja.

 

Bw. Mapunda amewasihi watumishi hao kutoka Ofisi za Kanda, Makao Makuu na Maduka ya MSD kuongeza juhudi katika kujifunza mambo mapya yaliyoboreshwa kwenye mfumo, ili kuboresha huduma kwa mteja.

 

“Tumieni fursa hii kujifunza mambo mapya yaliyohuishwa kwenye mfumo, najua mmekua mkitumia mfumo huu kwenye kazi zenu za kila siku, hakikisheni hamtumii changamoto za mfumo huu katika matendo yasiyofuta kanuni na taratibu. “Alisema Bw. Mapunda

 


44444.jpg
            
                                          Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA MSD Bi. Habiba Issa,

                                           Akitoa Mada Wakati wa Mafunzo ya TEHAMA

Naye Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA Bi. Habiba Issa amemshukuru Mkurugenzi Mkuu wa MSD kwa kukubali mafunzo hayo yafanyike, kwani yatasaidia kuwajengea uwezo watumishi kwenye maeneo mbalimbali yaliyoboreshwa

 

“Kuna vitu vingi vipya vimeogezwa kwenye mfumo ambavyo watumiaji wanatakiwa wafundishwe ili kuboresha utendaji wao na huduma kwa wateja wetu” Alisema Bi. Habiba.


77777777.jpg

                                 Watumishi wa MSD Wakifuatilia Mada Wakati wa Mafunzo ya TEHAMA

 

Mkurugenzi Mkuu NHIF Aipongeza MSD

PIC_4.jpg

Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw. Bernard Konga, ameipongeza MSD kwa kuboresha mfumo wake wa manunuzi ya vifaa vya maabara na vitendanishi vyake, kwa kwenda kununua vifaa hivyo moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji.

Ameongeza kuwa hatua hiyo itarahisha upatikanaji wa vifaa hivyo nchini na kupunguza gharama za huduma za vipimo vya kimaabara kwa wananchi.

 

PIC_1.jpg

Bw. Konga ametoa pongezi hizo alipotembelea Makao Makuu ya MSD kwa lengo la kuboresha uhusiano na ushirikiano wa kikazi baina ya MSD na NHIF, mathalani katika kuboresha huduma za kimaabara kwenye vituo vya kutolea huduma za afya chini.

 

Kwa upande wake Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi wa MSD Bw. Joseph Kitukulu, amesema gharama za vifaa hivyo na vitendanishi zimepungua kwa zaidi ya asilimi 50, ambapo vituo vya kutolea huduma za afya vya ngazi zote nchini wanaweza kuwa navyo.

PIC_2.jpg

 

Aliongeza kuwa vifaa hivyo ni pamoja na mashine ya kupima wingi wa damu, sukari na zile za kupima kiwango cha kemikali mwilini.

Aidha kwa upande wa mashine za kuchuja damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo, mashine zilizonunuliwa zitawezesha kushuka kwa gharama za uchujaji wa damu kwa wagonjwa hao kwa kiasi kikubwa.

Tayari vituo vya afya nchini vimeanza kununua mashine hizo kutoka MSD, huku wataalamu wa maabara wa MSD wakiendelea kukutana na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuzitambulisha mashine hizo na kujiridhisha kuhusu utendaji kazi wake.

 

PIC3.jpg


Mameneja wa Kanda za MSD Wanolewa

1.jpg

                        Mkurugenzi wa Rasilima Watu na Utawala wa MSD, Bw. Erick Mapunda akifungua

                                kikao cha tathimini kilichohusisha Mameneja wa Kanda wa MSD

 

Mkurugenzi wa Rasilima Watu na Utawala wa MSD, Bw. Erick Mapunda amewataka Mameneja wa Kanda za MSD kusimamia vyema utekelezaji wa majukumu yao ili kufikia lengo la taasisi katika utoaji wa huduma bora kwa Wananchi.

 

Bw. Mapunda ametoa rai hiyo leo wakati akifungua kikao kazi cha Memeneja wa Kanda wa MSD waliokutana MSD Makao Makuu kwa ajili ya tathmini ya utendaji ya mwaka wa fedha uliopita, pamoja na kuweka malengo mapya ya mwaka huu wa fedha.


2.jpg

                     Mameneja wa Kanda za MSD, Wakifuatilia mada wakati wa tathimini ya utendaji

Wataalamu Kutoka Muhimbili Watembelea MSD

Z3.jpg

                           

Baadhi ya madaktari na Wataalam wa baabara wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,Mloganzila

wametambulishwa mashine na vitendanishi vya maabara vipya vinavyonunuliwa na Bohari ya

Dawa(MSD) kwa matumizi ya vituo vya kutolea huduma za afya vya serikali nchini.

 

Z6.jpg

Mtaalam wa maabara wa MSD Joseph Kitukulu amewaeleza kuwa,mbali na vifaa

hivyo kutumia teknolojia ya kisasa, kupunguza muda na kuwa na gharama nafuu

vinauwezo wa kuchukua sampuli nyingi zaidi.

 

Z2.jpg

Kwa upande wake,Msimamizi wa Utekeleza Mpango Mkakati wa MSD, Bi. Neema

Mwale amesema kuwa hatua ya MSD kununua vifaa hivyo kutoka kwa wazalishaji

itachangia juhudi za serikali kuboresha huduma za afya za wananchi na kuipunguzia

serikali gharama kwa takribani asilimia 40 hadi 50.

 

 

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker