Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Yaipongeza MSD kwa Kupata Hati Safi ya Ukaguzi wa Hesabu Zake

EA183DD7-8E1F-4CCF-8505-4ECE49AC4CCC.jpeg

Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe.Naghenjwa Kaboyoka ameipongeza MSD kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu zake, na kuitaka kuendeleza rekodi hiyo safi kwa ustawi wa taasisi hiyo kiutendaji.

Ametoa pongezi hizo leo Kamati hiyo ilipokuwa ziarani MSD, ambapo ilipokea taarifa ya utendaji ambayo inafafanua mikakati ya maboresho ya utendaji wa MSD, mwenendo wa mapato na matumizi ya fedha na Mnyororo wa Ugavi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara.

Ameipongeza pia MSD kwa kuteuliwa kuwa mnunuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na kusema kuwa hiyo ni heshima kubwa kwa Taifa.

287978CA-DC65-4294-A262-D3E7E858A3CB.jpeg

Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Dkt. Fatma Mrisho ameihakikishia Kamati hiyo kuwa, pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili MSD bado inaendelea kutoa huduma bora na za kiwango cha juu kwa wananchi na kusimamia mnyororo wa ugavi ili kuleta tija kwenye mfumo wa afya wa nchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean R. Bwanakunu amesema MSD inajipanga sasa kuhakikisha inafanyia kazi maoni na

maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na kamati hiyo kwani ni maelekezo yenye lengo la kuiboresha MSD, ili izidi kutimiza majukumu yake ya kila siku

kwa ufanisi katika kuwahudumia wananchi.

87AA4840-2F96-472A-8DE6-5DC7D148B3F7.jpeg

MSD na SADC Wajadili Muongozo wa Manunuzi ya Pamoja ya Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi

 

 

 

 

626963FD-CE3A-41E5-B318-3000BD2C6C78.jpeg

Bohari ya Dawa (MSD) kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imeratibu Mkutano wa wataalamu wa manunuzi ya pamoja (SADC Pooled Procurement Services (SPPS) unaofanyika jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ilikuwa ni kupitia mwongozo wa manunuzi wa pamoja wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi wanachama wa SADC. 

Akifungua mkutano huo, Mfamasia Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Bw. Daudi Msasi amewashukuru wawakilishi wa nchi wanachama wa SADC kwa kuitikia wito wa kushiriki kwenye mkutano huo na kwa kuiamini Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa za pamoja. 

Aidha Bw. Msasi pia ameeleza kuwa MSD imekuwa miongoni mwa taasisi bora barani Afrika zinazo shughulika na mnyororo wa ugavi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara. 


3CDE457D-B3FD-4B16-A9ED-2E12224BDA1C.jpeg

 

 

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Manunuzi wa MSD Bw. Abdul Mwanja amesema MSD imejipanga kuanza utekelezaji wa jukumu hilo na tayari imeshatekeleza jukumu hilo kama lilivyoainishwa katika Hati ya Makubaliano na Sekretariati ya SADC (MoU) kwa kuanzisha kitengo kitakachoshughulikia manunuzi hayo kwa upande wa SADC. 

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema, faida ambazo nchi wanachama wa SADC watazipata ni pamoja na kupata dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa bei nafuu na vyenye ubora, kuboresha kiwango cha usambazaji kwa kila nchi mwanachama. 


CAB58CBD-363C-4E50-B6D1-BFE8B3E18AA6.jpeg

 

Ameongeza kuwa kupatikana kwa fursa hii ni heshima kubwa kwa Tanzania, hatua ambayo italeta ushirikiano ndani ya kanda na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, pia kuongeza fursa uwekezaji wa viwanda vya kuzalisha dawa na vifaa tiba kwa nchi za SADC na nje, hivyo kupanua soko.

 

Tanzania kupitia MSD ilishinda zabuni ya kuwa mnunua wa pamoja wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa niaba ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

 

1DF4DD23-E561-4819-A056-047319435CC2.jpeg

Tanzania Yatoa Msaada wa Dawa, Vifaa Tiba na Chakula

2C960A10-A632-46B2-AC3A-495762E3C5D8.jpeg

 

 

 

Serikali ya Tanzania imetoa msaada wa Dawa na Vifaa Tiba na vyakula kwa nchi tatu za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe kufuatia kimbunga cha IDAI kilichotokea hivi karibuni kwenye nchi hizo. Kimbunga hiko kimesababisha maafa ya watu kadhaa huku wengine wakikosa makazi.

 

Wakizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof.  Palamagamba Kabudi na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi a, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wamesema msaada huo ni agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean R. Bwanakunu amesema dawa na vifaa tiba vyote vilivyotolewa havitaathiri upatikanaji wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za Afya nchini,kwani dawa zipo za kutosheleza mahitaji ya nchi.

 

Naye Mkuu wa Mafunzo na Utendaji wa Kivita Kamandi ya Jeshi la Anga Brigedia Jenerali Francis Shirima ambao ndio wamepewa kazi ya kusafirisha msaada huo na Serikali amesema kazi hiyo itafanyika leo na kuwafikia walengwa kama ilivyooagizwa.

 

Kwa upande wao mabalozi wanaoziwakilisha nchi hizo hapa nchini, Balozi wa Msumbiji, Bi.Monica Mussa, Glad Chembe Munthali- Balozi wa  Malawi na Martine Tavenyika - wa  Zimbabwe wameshukuru kwa msaada huo na kusema Tanzania imeonyesha dira ya ushirikiano mwema.

MSD na SADC Wakutana Kujadili Muongozo wa Manunuzi ya Pamoja ya Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi

 

 

 

626963FD-CE3A-41E5-B318-3000BD2C6C78.jpeg

Bohari ya Dawa (MSD) kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imeratibu Mkutano wa wataalamu wa manunuzi ya pamoja (SADC Pooled Procurement Services (SPPS) unaofanyika jijini Dar es Salaam. Lengo la mkutano huo ilikuwa ni kupitia mwongozo wa manunuzi wa pamoja wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi wanachama wa SADC. 

Akifungua mkutano huo, Mfamasia Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Bw. Daudi Msasi amewashukuru wawakilishi wa nchi wanachama wa SADC kwa kuitikia wito wa kushiriki kwenye mkutano huo na kwa kuiamini Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa za pamoja. 

Aidha Bw. Msasi pia ameeleza kuwa MSD imekuwa miongoni mwa taasisi bora barani Afrika zinazo shughulika na mnyororo wa ugavi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara. 


3CDE457D-B3FD-4B16-A9ED-2E12224BDA1C.jpeg

 

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Manunuzi wa MSD Bw. Abdul Mwanja amesema MSD imejipanga kuanza utekelezaji wa jukumu hilo na tayari imeshatekeleza jukumu hilo kama lilivyoainishwa katika Hati ya Makubaliano na Sekretariati ya SADC (MoU) kwa kuanzisha kitengo kitakachoshughulikia manunuzi hayo kwa upande wa SADC. 

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema, faida ambazo nchi wanachama wa SADC watazipata ni pamoja na kupata dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa bei nafuu na vyenye ubora, kuboresha kiwango cha usambazaji kwa kila nchi mwanachama. 


CAB58CBD-363C-4E50-B6D1-BFE8B3E18AA6.jpeg

 

Ameongeza kuwa kupatikana kwa fursa hii ni heshima kubwa kwa Tanzania, hatua ambayo italeta ushirikiano ndani ya kanda na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, pia kuongeza fursa uwekezaji wa viwanda vya kuzalisha dawa na vifaa tiba kwa nchi za SADC na nje, hivyo kupanua soko.

Tanzania kupitia MSD ilishinda zabuni ya kuwa mnunua wa pamoja wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa niaba ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

1DF4DD23-E561-4819-A056-047319435CC2.jpeg

Wajumbe wa Bodi na Menejimenti ya Bohari ya Dawa ya Taifa ya Uganda Waitembelea MSD

DAF269B6-55E5-4BCC-9C47-667A100E3338.jpeg


 

Wajumbe wa Bodi na Menejimenti ya Bohari ya Dawa ya Taifa, nchini Uganda (NMS) wametembelea Bohari ya Dawa (MSD) kubadilishana uzoefu na kujifunza namna MSD inavyoshirikiana na Mfuko wa Bima ya Afya nchini (NHIF).

Pamoja na mambo mengine Meneja Mkuu wa NMS Bwana Moses Kamabare ameipongeza MSD kwa kuboresha utendaji wake ikiwa ni pamoja na huduma zake kwa wateja na kufanya mabadiliko makubwa katika mnyororo wa ugavi.

Akizungumza na ugeni huo,Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Dkt. Fatma Mrisho amesema ushirikiano wa taasisi hizi mbili ni muhimu sana,hasa kwenye eneo la kubadilishana uzoefu kiutendaji, kwa nia ya kuboresha huduma.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema MSD imefanya maboresho makubwa kiutendaji,na ni siri kubwa ya mafanikio katika kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker