Mhe. Ummy Mwalimu, Azindua Bodi Mpya ya Wadhamini ya MSD.

 

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_17.06.42_1.jpeg

Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu, Akiwa kwenye Picha ya Pamoja na

Wajumbe Wapya wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Mara baada ya

Kuitambulisha Mbele ya Waandishi wa Habari.

 

  

DAR ES SALAAM:

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo amezindua Bodi mpya ya Wadhamini ya Bohari

ya Dawa (MSD) na kuwaelekeza wajumbe hao Bodi kuhakikisha wanawezesha kuboresha

upatikanaji wa bidhaa za afya zenye ubora na bei nafuu.

 

Waziri Ummy amewaeleza wajumbe hao wa Bodi ya Wadhamini kuwa watapimwa kwa

kuangalia hali halisi ya upatikanaji wa bidhaa za afya kwenye vituo vya kutolea huduma

za afya nchini.

 

Pia, amewasisitiza kuhakikisha katika majukumu yote ya MSD wanazingatia sheria,

kanuni na taratibu zote za ununuzi wa umma, ili kuleta ufanisi na tija katika utendaji,

sambamba na kuondoa hoja za ukaguzi.

 

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_19.33.51.jpeg 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Bi. Rosemary

Silaa amewataka watumishi wa MSD kubadilika na kutekeleza majukumu

yao kwa kuzingatia weledi, ili kubadili taswira iliyojengeka juu ya utendaji

usioridhisha wa taasisi hiyo.

  

Wajumbe hao ni pamoja na Bi.Rosemary Silaa ambaye ni Mwenyekiti, Dkt. Julius Mwaiselage,

Dkt.Ntuli Kapologwe, Meshack Anyingisye, Rehema Katuga, John Mathew Mnali, Dkt. Mwamvita Kissiwa, Dkt. Danstan Hipolite Shewiyo na Brenda Msangi.

 

Bohari ya Dawa Msumbiji Yapongeza Juhudi za MSD Kuboresha Huduma, Pamoja na Ujenzi wa Viwanda

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_10.10.34_2.jpeg

Wajumbe Kutoka Bohari ya Dawa (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) Msumbiji, Wakiwa kwenye Picha ya Pamoja na Uongozi wa Bohari ya Dawa (MSD), Mara Baada ya Kutembelea Makao Makuu ya MSD Kwa Lengo la Kubadilishana Uzoefu. 

 

  

DAR ES SALAAM:

Ujumbe kutoka Bohari ya dawa (CMAM) na Mamlaka ya Dawa

na Vifaa Tiba (ANARME) Msumbiji leo wametembelea MSD

Makao Makuu kwa lengo la kujifunza na kubadirishana uzoefu.

 

Ujumbe huo Msumbiji ulifanya ziara ya kutembelea maghala ya kuhifadhia

bidhaaza afya ya MSD pamoja na kiwanda cha kuzalisha barakoa na kiwanda

cha kuzalisha vidonge KPI.

  

Ujumbe huo umevutiwa na hatua ya MSD kuongeza jukumu la kuzalisha

bidhaa za afya ambazo zinasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama

za kuagiza bidhaa hizo kutoka nje.

  

Aidha, pamoja na mambo mengine ujumbe huo ulikutana na Kurugenzi

za Ugavi na TEHAMA na kupata maelezo namna mifumo mbalimbali

inavyofanya kazi katika mnyororo wa ugavi na kuahidi kuiga mazuri punde

tu warejeapo nchini kwao.

 

 Katika hatua nyingine ujumbe huo ulipata fursa ya kutembelea wateja

wa MSD ambao ni hospitali ya Mifupa, MOI na Taasisi ya Moyo (JKCI)

kwa lengo la kujifunza namna taasisi hizo zinavyoendesha shughuli

zake.

 

 

MSD Yapongezwa kwa Mageuzi ya Huduma, ndani ya Muda Mfupi.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_10.10.34.jpegMganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makorora mkoani Tanga, Dkt.Angelina Meshack, Akiongea na Waandishi na Ujumbe Maalum Kutoka MSD (Hawapo Pichani) Walipomtembelea Ofisini Kwake, Kupata Mrejesho wa Huduma Zitolewazo na Bohari ya Dawa (MSD)

 

TANGA:

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makorora mkoani Tanga, Dkt.Angelina Meshack

ameipongeza serikali kupitia MSD, baada ya kupokea vifaa vya chumba cha

upasuaji ikiwemo kitanda cha upasuaji, mashine ya dawa ya usingizi na taa

zinazotumika wakati wa upasuaji amesema vifaa hivyo ni msaada mkubwa

katika kituo hicho kwani awali kulikuwa na changamoto kwenye hutoaji huduma.

 

"Awali tulikuwa hatufanyi upasuaji kabisa kwa hiyo tulivyopokea fedha

kwa ajili ya ukarabati majengo ya kufanyia upasuaji tulifanya hivyo na

baadae vifaa vililetwa na MSD na kuanza kutoa huduma za upasuaji".

Amesema Dkt.Angelina

 

Amesema baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo walianza kutoa huduma ya

upasuaji mbalimbali wa mama wajawazito pamoja na upasuaji mdogo

kwani hapo awali walikuwa wanawapeleka wagonjwa hospitali ya Bombo

kwa sababu huduma hiyo haikuwepo hapo kituoni.



"Kwa ujio wa vifaa hivi imerahisisha mama mjamzito akipata changamoto

moja kwa moja tunaweza kumpa huduma ya upasuaji na tunaokoa

maisha ya mama pamoja na kichanga". Amesema.

 

Pamoja na hayo Dkt.Angelina amesema walikabidhiwa pia na jenereta kwa ajili

ya hospitali hiyo lakini wakaamua kuwasiliana na ofisi ya mganga mkuu ili

waweze kuichukua na kuikabidhi kwenye vituo vingine ambavyo havina jenerata

kwa sababu kituo hicho kilikuwa na jenerata ambayo walikuwa wameshanunua awali.

 

Ameeleza kuwa hali ya upatikanaji wa dawa katika kituo hicho ni nzuri kwani

kwa sasa dawa muhimu zinapatikana kwa asilimia 90 na wanaendelea kutoa

huduma bora kwa wananchi

                                    

 

UNFPA Yatoa Msaada wa Dawa za Uzazi wa Mpango kwa Serikali ya Tanzania

 

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_10.10.34_1.jpegUjumbe Maalum Kutoka UNFPA, Ukiwa Kwenye Picha ya Pamoja na Uongozi wa MSD, Mara Baada ya Kutembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa, Yaliyoko Keko jijini Dar es Salaam .

 

 

DAR ES SALAAM:

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshugulikia Afya ya Uzazi

na Idadi ya Watu UNFPA limeikabidhi Serikali ya Tanzania

msaada wa dawa za uzazi wa mpango.

 

Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika Bohari ya Dawa (MSD)

Mwakilishi wa UNFPA nchini Tanzania Bw. Mark Bryan Schreiner

amesema msaada huo ni sehemu ya jitihada za UNFPA kuisaidia

Serikali ya Tanzania kuboresha huduma za uzazi wa mpango

kwa wananchi.

 

Ameongeza kuwa Tanzania imekuwa mshirika mkubwa wa UNFPA

katika utekelezaji na uboreshaji wa huduma za uzazi wa mpango

jambo ambalo linachagiza katika stawisha afya za wananchi

hasa wa hali ya chini.

  

Naye mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Felix Bundala

ameishukuru UNFPA kwa kuendeleza ushirikiano mzuri uliopo

kati yake na Tanzania hasa katika kuisaidia Tanzania kwenye

nyanja mbalimbali za uboreshaji wa huduma za afya.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai

amesema MSD imepokea dawa hizo na jukumu la MSD ni

kuhakikisha zinafika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya

nchini, lengo likiwa kuboresha huduma za afya hasa ya mama

na mtoto.

 

 

 

 

                                    

 

Kamati ya Afya Bunge la Zambia, Yaipongeza MSD kwa Maboresho ya Utendaji na Ujenzi wa Viwanda

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_14.21.00.jpeg

Kamati ya Bunge ya Afya, Maendeleo na Huduma za Jamii ya Bunge la Zambia Ikiwa kwenye Ziara ya Kutembelea Viwanda vya MSD.

 

 DAR ES SALAAM:

Kamati ya Bunge ya Afya, Maendeleo na Huduma za Jamii,ya Bunge la Zambia

wamevutiwa na hatua ya Bohari ya dawa (MSD) kuanza kuzalisha baadhi ya

bidhaa za afya kwa kutumia wataalam wake wa ndani.

Hayo yamebainishwa hii leo, tarehe 26/5/2022 baada ya Kamati hiyo ya Afya

kutoka Zambia, kuitembelea MSD kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu

katika masuala yanayohusu mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_14.20.28.jpeg

Akizungumza kwaniaba ya ujumbe huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge ya Afya,

Maendeleo na Huduma za Jamii, ya Bunge la Zambia, Mhe.Dkt. Christopher K. Kalila

amesema wamevutiwa na hatua ya Bohari ya dawa (MSD) kuanza kuzalisha baadhi

ya bidhaa za afya kwa kutumia wataalam wake wa ndani.

 

Mhe.Dkt. Kalila ameongeza kuwa MSD Tanzania ni kama pacha wa Bohari ya Dawa

ya nchini Zambia, kwani sheria yao pia imefanyiwa mabadiliko na kuiwezesha Bohari

hiyo kuanza kuzalisha bidhaa za afya.

 

"Ni vyema taasisi zetu hizi mbili zikawa karibu ili kubadilishana uzoefu, na utaalamu

katika maeneo mabalimbali ili kusukuma kwa pamoja ajenda ya uanzishaji wa viwanda

vya bidhaa za afya na kuondoa utegemezi wa bidhaa kutoka nje sambamba na kupunguza

gharama." Alisema Dkt. Kalila.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_14.20.27.jpeg

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai amesema

kwa pamoja na nchi nyingine kama Zambia yanaweza kufanyika mazungumzo

ya pamoja ya kuwezesha ununuzi wa pamoja wa bidhaa za afya, kupitia mpango

wa manunuzi ya pamoja ya SADC unaoratibiwa na MSD kwa nchi 16, kwa

kupitia mpango huo, nchi wanachama zitanufaika, sambamba na kupaisha soko

la viwanda vya ndani.

 

Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na mambo mengine wametembelea viwanda vya

MSD vya kuzalisha barakoa, pamoja na kiwanda cha dawa cha Keko Pharmaceuticals,

kinachosimamiwa na MSD.

                                              

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker