MSD Yashinda Tuzo za Mwajiri Bora Tanzania

dadaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.jpg

                                

 

 

Dar es Salaam. 

 

Taasisi ya Serikali inayojihusisha na ununuziutunzaji na usambazaji dawavifaatiba 

na vitendanishi vya maabara nchini Bohari ya Dawa (MSD) imeshindatuzo 2 za Mwajiri 

bora za ATE (Association of Tanzania Employers) kwamwaka 2019.

 

Pamoja na kushinda tuzo hizo zilizofanyika Serena Hotel Desemba 18, MSD imeingia

kwenye nafasi ya kumi bora kwamwajiri bora Tanzania kwa kushika nafasi ya sita na 

kuwa miongoni mwa taasisi chache za umma zilizoshinda.

 

Tuzo hizo ni pamoja na mwajiri bora katika utumishi wa umma(overall public sector

employer), mwajiri bora anayeangalia usawa wa maisha ya kazi (work life balance)

na mshindi wa pili kipengele cha mwajiri bora wa kizalendo (local employer).

 

Katika tuzo ya mwajiri bora katika utumishi wa ummanafasi ya mshindi wa pili

 imekwenda kwa Huduma za Mawasiliano ya Simu nchini (TTCL) na nafasi ya tatu

imekwenda kwa Benki ya Posta Tanzania (TPB Bank Plc).

 

Katika taasisi na mashirika yaliyoingia nafasi 10 bora kwa tuzo hizo mwakahuu ni pamoja na kampuni ya bia (TBL) iliyoshika nafasi ya kwanza, Geita Gold Mining Limited, Puma Energy Tanzania Limited, TPC Limited, Cocacola Kwanza Limited, Bohari ya Dawa (MSD), Exim Bank (T) Limited, Standard Chertered Bank, Songas Limited na Vodacom Tanzania 

iliyoshika nafasi ya 10.

 

AkizungumziaushindihuoMkurugenziMkuu waMSD BwLaureanRugambwaBwanakunu,

 ameishukuruBodi ya wadahamini ya taasisihiyomenejimentipamoja na wafanyakazi

wotekwamafanikiohayokwaniumoja na ushirikianowao katika majukumu ya kila siku

 ndioumepelekeawawezekuibukawashindi.

 

Aidha amewasihi kuongeza juhudi katika utekelezaji wa majukumu yao ili mwaka ujao (2020) taasisi hiyo iweze kujinyakulia ushindi mwingi zaidi ya mwaka huuAmeongeza kuwa mwisho watuzo hizo ndio mwanzo wa tuzo nyiginehivyo ni vyema kujipanga kwaajili ya mwaka Mpya.

 

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa RasilimaliWatu wa Taasisi hiyo ndugu.  

Frankie Nkoneamesema ushindi huo umetokana na ushirikiano madhubuti kati ya 

wafanyakazimenejimentiwizara katika utekelezaji wa mzuri wa mpango mkakati 

wa MSD, pamoja na mahusiano mazuri na chama cha wafanyakazi.

 

Naye Kaimu Meneja wa Rasilimali Watu wa MSD Bi.Siku Baleja ameonyesha kufurahia ushindi huoambapo licha ya kuwapongeza wafanyakazi wenzake kwa ushindiamebainisha kwamba anatazamia mwaka ujao MSD itashinda tuzo nyingi zaidikwani wana kila sababu na vigezo vyakuwa washindi.

 

 

 

Makamu wa Rais Aipigia Chapuo MSD Kusambaza Dawa SADC

samia.jpg

                                ,

 
Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa,

Bohari ya Dawa (MSD) imejipanga
vizuri kuhakikishajukumu la manunuzi ya

dawa ya pamoja kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya nchi zilizoko
Kusini

mwa Afrika (SADC)linatekelezwa kwa ufanisi.

 

                              Makamu wa Rais ameyasema hayo leo Alhamisi Novemba 7, 2019

                            wakati akifungua Mkutano wa mawaziri wanaoshughulikia sekta ya

                    afya na UKIMWI kutokanchi 16 wanachama uliomalizika leo, jijini Dar es Salaam.

 

                         Amesisitiza kuwa MSD kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha

                      mchakato huo, kwa kusaini mikataba na wazalishaji baada ya kutangaza zabuni.

 

bw.kunu.jpg

           

                             “Ninapenda kuwadhibitishia kwamba MSD imejipanga vizuri kuhakikisha

                            jukumu hili la uratibu wa manunuzi ya pamoja linatekelezwa kwa ufanisi

                        na kwamba hivi sasa taasisi hiyo inaendelea na kusaini mikataba na wazalishaji

                                         wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi,” alisema Samia

 

                            Ameongeza kuwa Serikali imejenga kiwanda cha kutengeneza dawa

                        ya viuadudu chenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 6 kwa mwaka na kwamba

                  dawa zinazozalishwa zinatumika kudhibiti wadudu dhurifu wakiwemo viluwiluwi vya

                                                        mbu wanaosababisha malaria.

 

mkutano_samia.jpg

    

                   “Nitumie fursa hii kuhamasisha nchi za SADC zinunue dawa ya viuadudu inayozalishwa

                    na kiwanda hiki kilichoko nchini kupitia utaratibu wa manunuzi ya pamoja wa nchi za

                                         SADC unaoratibiwa na Bohari ya Dawa MSD,” amesema.

 

 

                         Novemba mwaka 2017 Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) ilishinda zabuni ya

                            usambazaji wa dawa kwa nchi za SADC jukumu ambalo ilipewa na mkutano wa

                                         mawaziri wa afya na UKIMWI kutoka nchi wanachama.

 

 

                   Mchakato wa kusaini mikataba unaenda sambamba na kutoa mafunzo kwa watendaji

                      kutoka nchi wanachama juu ya namna ya kutumia mfumo wa kielektroniki wa

                    uagizaji wa dawa, ambao MSD unautumia katika uagizaji, ununuzi na usambazaji.

 

 

                                  Aidha mawaziri hao watapata fursa kuitembelea MSD siku ya  kesho

                                           Ijumaa Tarehe 7, 11, 2019 ili kujionea utendaji wake.

 


 

 

DKT. Shein Amwaga Pongezi kwa MSD.

DKT_SHEIN.jpg3.jpg

                          Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi

                    Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein ameipongeza MSD kwa kuteuliwa

                           kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa ajili ya nchi za SADC.

 

                                Dkt. Shein alimweleza hayo Mkurugenzi Mkuu wa MSD

                        Laurean Bwanakunu alipotembelea banda la MSD katika maonesho

                                  ya viwanda yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

 

                  Kingozi huyo pia ameishauri MSD kuwatembelea wazalishaji wakubwa

                       wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara wa mataifa

                     ili wapate taarifa sahihi na kuwashirikisha kuhusu MSD kuteuliwa

                        kusimamia manunuzi ya pamoja ya dawa kwa nchi za SADC.

 

                           DKT_SHEIN.jpg                               

                          

                     Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu

                   amesema tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya manunuzi ya pamoja,

                   ambapo tayari wameanza mchakato wa kupata wazabuni na kuanzisha

                mfumo wa kielektroniki utakaotumiwa na nchi wanachama kuleta mahitaji.

 

               Bohari ya Dawa MSD, ni moja ya taasisi zilizoshiriki maonyesho ya biashara

              na viwanda ya SADC yaliyofanyika wakati wa wiki ya mkutano wa SADC 2019,

                   katika viwanja vya kimataifa vya Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

Mawaziri wa Afya wa SADC Waitembelea MSD

4.jpg

                                 (Mawaziri wa Afya kutoka nchi za SADC wakimakinikia mada, mara walipotembelea MSD)

               Mawaziri kutoka Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Africa

                (SADC) wanaoshughulikia masuala ya Afya na Ukimwi

           wametembelea Ofisi za Bohari ya Dawa (MSD) zilizoko Keko,

                  jijini Dar es Salaam nakushuhudia jinsi mnyororo

                            mzima wa ugavi unavyofanya kazi.

 

                 Mawaziri hao wameonyesha kuridhishwa na kufurahishwa

                   na jinsi MSD ilivyojipanga katika kutekeleza majukumu

               yake kwa ufanisi,mathalani ununuzi, uhifadhi, na usambazaji

                     wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara huku

              wakibainishakuwa ni mfano wa kuigwa kwa nchi wanachama.

3.jpg

                     (Mawaziri wa Afya kutoka nchi za SADC wakimakinikia mada,

                                mara walipotembelea Bohari ya Dawa (MSD))

        Mawaziri hao wanaoshughulika na afya wameambatana na mwenyeji

             wao Waziri wa afya wa Tanzania, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb),

               ambaye amewaeleza waandishi wa habari utayari wa MSD

                 katika katika kufanya manunuzi ya pamoja kwa nchi

              za SADC na mchakato mzima uliopelekea MSD kupewa

                                              zabuni hiyo.

 

 

                 Aidha, amebainisha kuwa lengo la ziara hiyo ya Mawaziri

                 ni kuangalia uwezo, vifaa na utaalamu wa MSD katika

                     kutekeleza majukumu hayo kwa nchi wanachama.

 

index2.jpg

                           (Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean Bwanakunu, akitoa mada)

               Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean             

             Bwanakunu, ametoa tathimini ya ulipofikia mchakato mzima

          wa manunuzi ya pamoja, kwa nchi wanachama hadi sasa (SPPS),

             ambapo amebainisha kwamba wamekwisha pata wazabuni

                     na sasa mikataba iko kwa Mwanasheria Mkuu

                                 ikifanyiwa upembuzi, (Vetting).

 

 

               Aidha amewahakikishia mawaziri hao kutoka SADC kuwa

        mchakato wa manunuzi ya pamoja utapunguza gharama kwa kiasi

      kikubwa kwa nchi wanachama na kukuza uchumi wa viwanda kupitia

                                     uwekezaji wa viwanda vya dawa.

 

 

               Mawaziri hao kutoka SADC, walipata fursa ya kutembelea

              magahala ya kuhifadhia dawa ya MSD na kujionea jinsi kazi

               mbalimbali za utunzaji na ugavi, zinavyofanyika kwa weledi

                                         na ufanisi mkubwa.

 

index.jpg

(Meneja Mradi Msonge wa MSD Bw. Bill Singano, akitoa ufafanuzi mbele ya mawaziri wa Afya wa SADC)
 

MSD Yawasilisha Msaada wa Dharura kwa Majeruhi wa Ajali ya Moto Mkoani Morogoro

MOROGORO_CSR.jpg

                                ,

 

      

                                         Timu ya MSD ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD

                                Bw. Laurean Bwanakunu wakiwa sambamba na Mganga Mkuu wa Serikali

                                   Prof. Mohamed Kambi, wamewatembelea majeruhi wa ajali ya moto,

                                iliyosababishwa na mlipuko wa lori la mafuta waliolazwa katika hospitali

                                                             ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

 

                                                                MOROGORO_CSR.jpg4.jpg

 

                                 Pamoja na kuwajulia hali majeruhi hao, ujumbe huo pia ulilenga

                               kufuatilia na kufahamu misaada ya haraka ya kitabibu inayohitajika

                                            kwa sasa hospitalini hapo ili kusaidia majeruhi.

                                                              MOROGORO_CSR.jpg3.jpg

 

                          Aidha, Bohari ya Dawa imechukua jitahada za makusudi kwa kusafirisha

                                shehena hiyo kutoka kwenye magahala yake jijini Dar es salaam,

                                                  ili kuokoa maisha ya watanzania wenzetu.

 

 

 

 


 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker