MSD Yashinda Tuzo za Mwajiri Bora Tanzania
Dar es Salaam.
Taasisi ya Serikali inayojihusisha na ununuzi, utunzaji na usambazaji dawa, vifaatiba na vitendanishi vya maabara nchini Bohari ya Dawa (MSD) imeshindatuzo 2 za Mwajiri bora za ATE (Association of Tanzania Employers) kwamwaka 2019.
Pamoja na kushinda tuzo hizo zilizofanyika Serena Hotel Desemba 18, MSD imeingia kwenye nafasi ya kumi bora kwamwajiri bora Tanzania kwa kushika nafasi ya sita na kuwa miongoni mwa taasisi chache za umma zilizoshinda.
Tuzo hizo ni pamoja na mwajiri bora katika utumishi wa umma(overall public sector employer), mwajiri bora anayeangalia usawa wa maisha ya kazi (work life balance) na mshindi wa pili kipengele cha mwajiri bora wa kizalendo (local employer).
Katika tuzo ya mwajiri bora katika utumishi wa umma, nafasi ya mshindi wa pili imekwenda kwa Huduma za Mawasiliano ya Simu nchini (TTCL) na nafasi ya tatu imekwenda kwa Benki ya Posta Tanzania (TPB Bank Plc).
Katika taasisi na mashirika yaliyoingia nafasi 10 bora kwa tuzo hizo mwakahuu ni pamoja na kampuni ya bia (TBL) iliyoshika nafasi ya kwanza, Geita Gold Mining Limited, Puma Energy Tanzania Limited, TPC Limited, Cocacola Kwanza Limited, Bohari ya Dawa (MSD), Exim Bank (T) Limited, Standard Chertered Bank, Songas Limited na Vodacom Tanzania iliyoshika nafasi ya 10.
AkizungumziaushindihuoMkurugenziMkuu waMSD Bw. LaureanRugambwaBwanakunu, ameishukuruBodi ya wadahamini ya taasisihiyo, menejimentipamoja na wafanyakazi wotekwamafanikiohayokwani, umoja na ushirikianowao katika majukumu ya kila siku ndioumepelekeawawezekuibukawashindi.
Aidha amewasihi kuongeza juhudi katika utekelezaji wa majukumu yao ili mwaka ujao (2020) taasisi hiyo iweze kujinyakulia ushindi mwingi zaidi ya mwaka huu. Ameongeza kuwa mwisho watuzo hizo ndio mwanzo wa tuzo nyigine, hivyo ni vyema kujipanga kwaajili ya mwaka Mpya.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa RasilimaliWatu wa Taasisi hiyo ndugu. Frankie Nkone, amesema ushindi huo umetokana na ushirikiano madhubuti kati ya wafanyakazi, menejimenti, wizara katika utekelezaji wa mzuri wa mpango mkakati wa MSD, pamoja na mahusiano mazuri na chama cha wafanyakazi.
Naye Kaimu Meneja wa Rasilimali Watu wa MSD Bi.Siku Baleja ameonyesha kufurahia ushindi huo, ambapo licha ya kuwapongeza wafanyakazi wenzake kwa ushindi, amebainisha kwamba anatazamia mwaka ujao MSD itashinda tuzo nyingi zaidi, kwani wana kila sababu na vigezo vyakuwa washindi.
|