MSD Yatoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Vifaa Tiba na Maabara Nchini.

WhatsApp_Image_2022-09-19_at_13.26.53.jpegKaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD Bw.William Singano, Akiongea na Wataalamu wa Vifaa Tiba na Mabaara nchini, Wakati wa Kufunga Mafunzo, yaliyoendeshwa na MSD kwa Wataalamu Mkoani Morogoro.

  

Morogoro: 

Mafunzo ya siku tatu kwa wahandisi vifaa tiba na wataalam wa Maabara

nchini, yamefungwa leo mkoani Morogoro.

 

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa wakati mmoja kwa mikoa mitano kwa ajili ya wataalam

wa nchi nzima yalikuwa na lengo la kuwafundisha wataalamu wa usimikaji,

matumizi na ukarabati wa mashine za maabara na vifaa vinavyosambazwa

na MSD.

 

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD,

Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji Bw.William Singano amesema

mafunzo hayo ni muhimu kwa wahandisi vifaa tiba na wataalam wa maabara

kwa kuwa yanawawesha watumiaji hao kumudu kuzitumia, kuzitunza na

kuzifanyia ukarabati.

 

BW. Singano ameishuikuru Serikali kuboresha huduma za afya kwa kuwezesha

mashine na vifaa vya kisasa nchi nzima.

 

Mafunzo hayo yalitolewa mikoa ya Tabora, Morogoro, Mbeya, Kilimanjaro

na Mwanza ambapo wataalam kutoka mikoa mingine yote waliungana

kupata mafunzo hayo kwa pamoja.

Dkt. Mollel Aishauri MSD Namna ya Kuboresha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya Nchini.

WhatsApp_Image_2022-09-01_at_08.10.55.jpegNaibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel Akiongea Watumishi wa MSD, Mara baada ya Kutembelea Banda lao, Wakati Maonesho ya Kimataifa ya Wadau wa Bidhaa za Afya ya Afrika Mashariki, Yanayofanyika Jijini Dar es Salaam.

 

 

  

DAR ES SALAAM: 

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameishauri Bohari ya Dawa (MSD)

kutengeneza mpango wa muda mrefu wa kuzungumza na wazalishaji dawa

na bidhaa nyingine za afya kutoka nchi zinazozalisha bidhaa hizo, ili

kuja kuwekeza nchini Tanzania, hatua ambayo itarahisisha upatikanaji

wa bidhaa za afya nchini.

 

 

Naibu waziri ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa maonesho ya

Kimataifa ya wadau wa bidhaa za afya ya Afrika Mashariki

yaliyoanza leo jijini Dar es Salaam.

 

 

Ameongeza kuwa MSD pia iangalie namna ya kuingia mikataba na nchi

zinazozalisha bidhaa za afya kurahisisha kununua moja kwa moja kutoka

kwao, ili kupunguza gharama na kuwezesha kupata bidhaa za

kutosheleza mahitaji.

 

 

Kiongozi huyo pia amewahimiza wazalishaji hao wa nje kuja kuwekeza nchini

Tanzania kwa kuingia ubia na serikali.

 

 

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano MSD Bi. Etty Kusiluka,

 amemshukuru Dkt. Mollel kwa ushauri, na kuahidi kuufikisha kwenye Menejimenti ya

MSD ili uweze kufanyiwa kazi.

 

 

Aidha, ameendelea kuwakaribisha wananchi na wadau mbalimbali kutembelea banda la

MSD lilipo kwenye maonyesho hayo, ili waweze kupata taarifa mbalimbali

zinazohusiana na MSD, sambamba na kufahamu namna taasisi hiyo

inavyotekeleza majukumu yake.

 

 

Maonyesho hayo ya Kimataifa ya bidhaa za afya ya Afrika Mashariki yanafanyika

kwa siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee, ulioko jijini Dar es Salaam,

kwa kuwakutanisha Wadau kutoka nchi mbalimbali.

Usambazaji wa Vifaa vya CEmONC, Mikoa ya Dodoma na Singida

IMG-20220822-WA0119.jpg

             Vifaa vya CEmONC Vikiwa Vimesambazwa na MSD Kwenye Moja ya Kituo

Cha Afya Mkoani Singida.

 

  

DODOMA:

Bohari ya Dawa (MSD), kupitia Kanda yake ya Dodoma inayohudumia Mikoa

ya Singida na Dodoma imeendelea na zoezi la usambazaji wa vifaa vya

huduma ya dharula ya mama na mtoto (Comprehensive Emergency Obstetric

and New Born Care Services – CEmONC). 

 

Akizungumzia usambazaji huo Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma

Ndg. John Sipendi,amesema usambazaji wa vifaa hivyo kwenye

vituo vya kutolea huduma za Afyavinavyohudumiwa na Kanda yake ya

Dodoma ni utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan

la kuboresha huduma za dharula za mama na mtoto.

 

Amebainisha kwamba kwa sasa Kanda yake inatekeleza usambazaji

kwenye vituo takribani 26 vya kutolea huduma za afya ambavyo

vilianishwa kwa ajili ya kupatiwa vifaa hivyo katika

Mikoa ya Singida na Dodoma.   

 

"Ikumbukwe kwamba Rais amekuwa akiweka wazi kuwa

moja ya vipaumbele katika serikali ya  awamu hii ya 6, ni kuhakikisha

inaboreshaji huduma, hususani zitakazopunguza vifo vya mama na mtoto

wakati wa kujifungua". Alisema Sipendi

 

Meneja Sipendi amesisitiza Kwamba, ataendelea kuhakikisha vifaa vyote

vinavyoletwa kutoka makao makuu vinasambazwa kwa wakati na haraka

kwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya vilivyoainishwa.

 

Hata hivyo, pamoja na usambazaji wa vifaa vya CEmONC, Kanda ya Dodoma

imeendelea pia na usambazaji bidhaa nyingine za afya kwenye vituo vya kutolea

huduma za afya takribani 685 vilivyopo katika Mikoa ya Singida na Dodoma.

 

MSD Yachangia Maboresho ya Huduma za Uzazi Visiwani Zanzibar

WhatsApp_Image_2022-08-30_at_09.45.30.jpeg

Kaimu Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam Bw. Nuru Mwagoka,Akipokea Cheti Kutoka Kwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar     Mhe. Dkt. Husein Ally Mwinyi Kufuatia Mchango MSD Kwenye Mbio za Hisani Zilizolenga Kuboresha Huduma za Uzazi

 

  

ZANZIBAR:

Bohari ya Dawa (MSD), imeshiriki mbio na matembezi
ya hisani kwa ajili kuchangia huduma za uzazi salama kwa mama
na mtoto, zilizoandaliwa na Shirika la AMREF,
visiwani Zanzibar.
 
Akizungumza wakati wa kuhitimisha mbio hizo zilizoanzia
viwanja wa Maisara- Mnazi Mmoja majira ya asubuhi,
Mgeni Rasmi wa Shughuli hiyo, Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Husein Ally Mwinyi,
amewapongeza washiriki wote ikiwemo MSD kwa kushiriki
tukio hilo la kihistoria kuchangia maboresho ya huduma za
uzazi salama visiwani humo.
 
WhatsApp_Image_2022-08-30_at_09.45.29.jpeg 
“Nawapongeza wananchi, makampuni na mashirika wote
kwa ujumla kwa kushiriki kwenu kwenye mbio hizi za kusaidia
huduma ya mama na mtoto". Alisema Dkt. Mwinyi. 
 
Rais Mwinyi ametoa wito kwa taasisi, makampuni na wadau
mbalimbali kuiga mfano wa AMREF, ili kusaidia huduma
mbalimbali visiwani humo.
 
Ameongeza kwamba Serikali yake itaendelea kushirikiana
kwa ukaribu na wadau wote wenye nia ya kuchangia
maendeleo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Kaimu
Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam, Bw. Nuru Mwangoka,
amesema MSD ni mdau wa karibu kwa serikali ya mapinduzi
ya Zanzibar hasa kupitia sekta ya afya, hivyo walivyopokea
wito wa kushiriki na kuchangia huduma za afya hawakusita
kufanya hivyo.
WhatsApp_Image_2022-08-30_at_09.45.301.jpeg
 
"Sisi MSD, ni washirika muhimu wa sekta ya afya Zanzibar
kwani tumekua tukifanya kazi zetu kwa ushirikiano na Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, hivyo tulivyopokea wito wa
kushangia huduma hizi za uzazi hatukusita kushiriki”
alieleza Bw. Mwangoka
 
Aliongeza kuwa MSD kwenye mbio na matembezi hayo ya hisani,
imeweza kuchangia vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha
huduma za uzazi salama, visiwani humo.
 
Aidha, amesema msaada huo umekwisha wasilishwa kwa uongozi
wa AMREF, ukisubiri kupelekwa kwenye vituo vya kutolea
huduma za afya.
 
Katika mbio na matembezi hayo, washiriki wote wameweza
kutembea na kukimbia mbio hizo na kumaliza ikiwemo Kilometa 5,
na Kilometa 10, ambapo zote zimemalizikia katika viunga
vya uwanja wa Amaani.

 

Serikali Kuendelea Kuunga Mkono, Ujenzi wa Viwanda vya Dawa na Vifaa Tiba vya MSD.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_20.07.50.jpeg

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu Akiongea Mbele ya Wananchi

wa Mji wa Mkambako (Hawapo pichani) Juu ya Hatua Ujenzi wa

Kiwanda cha Dawa na Vifaa Tiba, Wakati wa Ziara ya

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan

Mkoani Njombe

  

 

NJOMBE: 

Serikali imeahidi kuendelea na ujenzi wa Kiwanda cha uzalishaji wa dawa na vifaa tiba

kilichopo chini ya Bohari ya Dawa (MSD), huko Idofi Makambako,

Mkoani Njombe, ilikuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya

nchini sambamba na kuokoa matumizi ya fedha za kigeni.

 

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo, alipokua akitoa

salamu zake kwa wananchi wa Makambako mara baada ya kupewa nafasi ya

kuzungumza kwenye ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa Makambako - Njombe.

 

"Mheshimiwa Rais, hapa Makambako tunajenga kiwanda cha Dawa na Vifaa tiba

ambapo ujenzi wake hapo nyuma ulisimama kwakuwa tunarekebisha mambo

kadhaa, lakini sasa tunaendelea na ujenzi" amesema Waziri Ummy Mwalimu.

 

"Nimesimama hapa kuwahakikishia wana Makambako, serikali itaendeleza

na kukamilisha ujenzi wa kiwanda hiki, na tutaleta shilingi Billioni 17

kukamilisha ujenzi" Alisisitiza Mhe. Ummy Mwalimu.

 

Waziri Ummy amesema hadi sasa serikali imekwisha toa kiasi cha shilingi

Bilioni 18 ikiwa ni kwa ajili ya ujenzi pamoja na kununua baadhi ya mashine

na hadi kukamilika kwake, kiwanda hicho kitagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 35.

 

Aidha Waziri Ummy ameongeza kwamba, kiwanda hicho kitazalisha dawa

za vidonge, (tablets), dawa za maji (syrup), pamoja na mipira ya mikono (gloves),

huku kikitarajia kutoa ajira kwa watu zaidi ya 200.

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker