Mkurugenzi Mkuu NHIF Aipongeza MSD

PIC_4.jpg

Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw. Bernard Konga, ameipongeza MSD kwa kuboresha mfumo wake wa manunuzi ya vifaa vya maabara na vitendanishi vyake, kwa kwenda kununua vifaa hivyo moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji.

Ameongeza kuwa hatua hiyo itarahisha upatikanaji wa vifaa hivyo nchini na kupunguza gharama za huduma za vipimo vya kimaabara kwa wananchi.

 

PIC_1.jpg

Bw. Konga ametoa pongezi hizo alipotembelea Makao Makuu ya MSD kwa lengo la kuboresha uhusiano na ushirikiano wa kikazi baina ya MSD na NHIF, mathalani katika kuboresha huduma za kimaabara kwenye vituo vya kutolea huduma za afya chini.

 

Kwa upande wake Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi wa MSD Bw. Joseph Kitukulu, amesema gharama za vifaa hivyo na vitendanishi zimepungua kwa zaidi ya asilimi 50, ambapo vituo vya kutolea huduma za afya vya ngazi zote nchini wanaweza kuwa navyo.

PIC_2.jpg

 

Aliongeza kuwa vifaa hivyo ni pamoja na mashine ya kupima wingi wa damu, sukari na zile za kupima kiwango cha kemikali mwilini.

Aidha kwa upande wa mashine za kuchuja damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo, mashine zilizonunuliwa zitawezesha kushuka kwa gharama za uchujaji wa damu kwa wagonjwa hao kwa kiasi kikubwa.

Tayari vituo vya afya nchini vimeanza kununua mashine hizo kutoka MSD, huku wataalamu wa maabara wa MSD wakiendelea kukutana na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuzitambulisha mashine hizo na kujiridhisha kuhusu utendaji kazi wake.

 

PIC3.jpg


Wataalamu Kutoka Muhimbili Watembelea MSD

Z3.jpg

                           

Baadhi ya madaktari na Wataalam wa baabara wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,Mloganzila

wametambulishwa mashine na vitendanishi vya maabara vipya vinavyonunuliwa na Bohari ya

Dawa(MSD) kwa matumizi ya vituo vya kutolea huduma za afya vya serikali nchini.

 

Z6.jpg

Mtaalam wa maabara wa MSD Joseph Kitukulu amewaeleza kuwa,mbali na vifaa

hivyo kutumia teknolojia ya kisasa, kupunguza muda na kuwa na gharama nafuu

vinauwezo wa kuchukua sampuli nyingi zaidi.

 

Z2.jpg

Kwa upande wake,Msimamizi wa Utekeleza Mpango Mkakati wa MSD, Bi. Neema

Mwale amesema kuwa hatua ya MSD kununua vifaa hivyo kutoka kwa wazalishaji

itachangia juhudi za serikali kuboresha huduma za afya za wananchi na kuipunguzia

serikali gharama kwa takribani asilimia 40 hadi 50.

 

 

 

Matumizi ya Cheti cha Dawa Kilichoboreshwa

MSASI_PRESS.png

                                                   Mfamasia Mkuu wa Serikali, Bw. Daudi Msasi

Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi, amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa, Halmashauri, Waganga Wafawidhi na Wafamasia kote nchini Kuzingatia na kusimamia matumizi ya miongozo na nyenzo za usimamizi wa bidhaa za afya, ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa dawa vituoni.

 Bw. Msasi amesisitiza kwamba kutozingatia matumizi sahihi ya miongozo na nyenzo muhimu katika utunzaji na utoaji wa dawa, kumekuwa kukisababisha changamoto mbalimbali katika upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

 Bw. Msasi ametoa rai hiyo alipozungumza na waandishi wa habari kufafanua kuhusu matumizi ya cheti cha dawa kwa ngazi zote za kutolea huduma za afya nchini.

 Aidha, Bw. Msasi amevielekeza vituo vya kutolea huduma za afya nchini kuhakikisha vinanunua vitabu vya “Prescription” ya dawa vilivyoboreshwa kutoka MSD, na pale vinapokosena kwenye Bohari basi wapakue kutoka tovuti ya Wizara ya afya.

 

IMG_20210703_113328_284.jpg

                             Bw. Daudi Msasi akizungumza mbele ya waandishi wa habari

Ameongeza kuwa vitabu hivyo vya “Prescription” iliyoboreshwa vitaanza rasmi kutumika kuanzia julai 10, mwaka 2021, lengo likiwa ni kuwezesha kutunza kumbukumbu sahihi za matumizi ya dawa na kurahisisha ufuatiliaje wake.

Tayari Bohari ya Dawa (MSD), imekwisha chapisha jumla ya Vitabu vya “ Prescription” takribani elfu sitini na tano (65,000), vikingoja kusambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Dkt. Gwajima, Afanya Ziara MSD

DK_Gwajima.jpg

                                                   Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima leo tarehe 3 mwezi wa 7,2021, amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimentiya Bohari ya Dawa (MSD) Kwenye ukumbi wa Bohari ya Dawa ulioko Keko jiji Dar es salaam, lengo likiwa ni kuangalia namna gani ya kuboresha huduma na upatikanaji wa bidhaa za afya nchini.

 

Dkt. Gwajima licha ya kukutana na Menejimenti ya MSD katika kikao cha ndani, alitembelea kiwanda cha kuzalisha Dawa cha Keko (Keko Pharmaceutical) kilichopo jijini Dar es Salaam, kinachosimamiwa na Bohari ya Dawa (MSD).

 

Katika Ziara hiyo Dkt.Gwajima alijionea uzalishaji wa dawa ambapo hivi Sasa kinazalisha aina kumi za dawa, zikiwemo za maumivu aina mbili na nyingine 8 zikiwa ni dawa za kuua vimelea vya magonjwa ya kuambukiza (antibacteria/antibiotics).

waziri_Gwajima_na_Menejiment.jpg

                         Dkt. Dorothy Gwajima akiwa kwenye kikao cha ndani na Menejimenti ya MSD

Hatahivyo, licha ya kazi kubwa iliyofanyika kiwandani hapo, Dkt. Gwajima alitoa maelekezo mbalimbali kwa uongozi wa kiwanda hicho, kwaajili ya kuboresha utendaji, uzalishaji, na taarifa muhimu zinazohusu kiwanda hicho.

 

Katika hatua nyinine,Dkt. Gwajima alitembelea Maghala ya kuhifadhia dawa, yaliyoko Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD), Keko jijini Dar es Salaam, na kuijonea uhifadhi wa dawa, sambamba na changamoto mbalimbali zinazoikumba Bohari hiyo upande wa uhifadhi na kuagiza mabadiliko kwenye maeneo mbalimbali ili kuboresha huduma za usambazaji wa bidhaa za dawa nchini


KIWANDA_KEKO.jpg

Dkt. Dorothy Gwajima akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mej.Gen Gabriel Saul Mhidze

launch event for mass replacement campaign (MRC)

To ensure that Tanzania is free from Malaria, the National Malaria Control Program (NMCP)under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MOHCDGEC) has been spearheading the National Insecticide Treated Nets (NATNETS) Programme since 2000 by planning, implementing and managing of the scaling-up of Insecticide Treated Net (ITN) use in Tanzania.

Three mass replacement campaigns have been implemented since 2015 and the fourth one is under implementation with effect from February 2020. Due to its competency, experience, and its role in the health commodity supply chain in Tanzania, MSD was assigned by the MOHCDGEC to facilitate distribution of LLINs to 50 councils throughout Tanzania. A total of 7,097,565 LLINs are to be distributed to 50 selected councils in ten (10) regions namely; Mbeya, Njombe, Songwe, Rukwa, Iringa, Singida, Dodoma, Manyara, Tanga, and Kilimanjaro.

For successful distribution of the LLINs, NMCP under MOHCDGEC initiated the launching event for the Mass Replacement Campaign 2020. The launching event was successfully conducted on 28th May 2020 at Chunya district in Mbeya region by Hon.  Ummy Mwalimu (MP), Minister of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children.

During the launch, the Minister expressed a vote of thanks to the Global Fund (GF) for the support that aims at maintaining universal access of the population to Long-Lasting Insecticide Treated Nets (LLINs).The Hon Minister emphasized that an Insecticide-treated net (ITN) is a mosquito net that repels, disables and/or kills mosquitoes when they come into contact with insecticides on the netting material. She further explained that Malaria prevalence rate has decreased by 50% from 14.8% in 2015 to 7.3% in 2017. In the event, the Minister conveyed continuous gratitude on the Government’s commitment in this year’s MRC and mentioned the confidence of the Ministry in MSD for its role in distribution.

The Minister stated that, MSD shall distribute all LLINs to 50 councils in 10 regions as scheduled under the good leadership of the Major General Gabriel Saul Mhidze (Dr), the Director General of Medical Stores Department. On the same note, the Director General of MSD expressed MSD’s commitment towards efficient distribution of LLINs.

The Minister on behalf of the Government expressed appreciation towards toall individuals and organizations who are supporting and collaborating in implementing the LLINs mass replacement campaign in Tanzania. She insisted that the Government is grateful to the Global Fund, President’s Malaria Initiative, for the financial and technical support.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker