MSD Yaboresha Huduma za Kusafisha Damu-Tumbi

web_3.jpeg

Baadhi ya Vitanda na Mashine za Kisasa, Vikiwa Vimesimikwa Kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani- Tumbi, Kufuatia Maboresho ya Huduma ya Kuchuja Damu

 

PWANI

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani - Tumbi imeanza kutoa huduma mpya ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo. Huduma hii imeanza kutolewa baada ya Bohari ya dawa (MSD) kukamilisha kufunga  mashine za kisasa 10 za kusafisha damu baada ya kuboresha miundombinu ya kuwezesha huduma.

 

Hatua hiyo ni muendelezo wa maboresho ya huduma za afya nchini yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Afya.

 

Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Amani Malima amesema mpaka sasa tayari huduma imeshatolewa kwa wagonjwa watatu na huduma hiyo imefanikiwa kwa asilimia100.

 

Kwa upande wake Fundi Sanifu vifaa tiba wa MSD Ikunda Harrison amesema mbali na kufunga mashine hizi MSD ilitoa mafunzo kwa watoa huduma wa hospitali hiyo, ambapo  kwa sasa jukumu kubwa la MSD ni kuhakikisha vitendanishi vya mashine hizo vinaendelea kuwepo wakati wote ili kuepuka kukwamisha huduma

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Atembelea Kiwanda cha MSD-Idofi

web-1.jpeg

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Antony Mtaka, Akipokea Maelezo kuhusu Uzalishaji wa Kiwanda cha Mipira ya Mikono cha MSD- Idofi, kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa Mradi huo, Bi. Selwa Hamid.

 

 

 

NJOMBE

 

Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Antony Mtaka na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Njombe imetembelea kiwanda cha Bohari ya Dawa (MSD) cha kuzalisha mipira ya mikono kilichopo Idofi, Makambako ambacho ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 70.

Mhe.Mtaka amesema kiwanda hicho ni muhimu kwa sekta ya afya kwani kitapunguza matumizi ya fedha za kigeni kununua bidhaa hiyo nje ya nchi na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa mipira ya mikono nchini.

Mtaka aliiagiza MSD ikamilishe kiwanda hicho ili uzalishaji uanze ili wananchi wanufaike na mradi huo na kutafuta masoko nchi za SADC.

Mwenyekiti wa bodi ya Wadhamini ya MSD Rosemary Silaa amesema kiwanda hicho kitatoa ajira 200 huku Mkurugenzi Mkuu MSD Mavere Tukai akieleza kuwa uzalishaji wa mipira ya mikono kiwandani hapo unatarajiwa kuanza mwezi Julai mwaka huu.

Uzalishaji wa kiwanda hicho utaiwezesha MSD kukidhi mahitaji yake kwa asilimia 83.4 ya mahitaji ya mipira ya mikono nchini.

Kwa upande wake Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi amesema serikali kupitia Wizara ya Afya inaunga mkono uanzishwaji wa viwanda vya bidhaa za afya, na watahakikisha kiwanda hicho kinaanza uzalishaji.

Kiwanda hicho kitaokoa matumizi ya fedha za kigeni Bilioni 24 kwa mwaka ambazo zingenunua bidhaa hiyo nje ya nchi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Atangaza Neema Sekta ya Afya Nchini

WhatsApp_Image_2022-10-26_at_15.53.56.jpegWaziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Mkurgenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai(wapili kushoto), na Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini Togolani Edriss Mavura (wakwanza kulia) Wakiwa kwenye Picha ya Pamoja na Kiongozi wa Serikali ya Jimbo la Chungcheongbuck 

nchini Korea kusini.

  

KOREA KUSINI: 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan

amedhamiria kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kuwezesha

upatikanaji wa wataalam, dawa, vitendanishi na vifaa tiba.

Mheshimiwa Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Oktoba 26, 2022 baada ya

kushuhudia utiaji saini wa Makubaliano ya Ushirikiano baina ya Bohari

ya Dawa Tanzania (MSD) na Serikali ya Jimbo la Chungcheongbuck

nchini Korea kusini.

 

Akizungumza wakati wa tukio hilo, ambalo pia lilihudhuriwa na Gavana

wa jimbo la Chungcheongbuck, Mheshimiwa Majaliwa amesema “Tukio hili 

la utiaji saini wa makubaliano haya ni ishara kwamba sasa tunakwenda

kuimarika kwenye sekta ya dawa, mkataba huu kwetu ni muhimu kwa

kuwa tunahitaji kujiimarisha katika eneo la upatikanaji wa dawa na tafiti.”

Sehemu ya makubaliano katika mkataba huo ni kujadili na kuendeleza

mahusiano ya kibiashara katika nyanja za masoko ya bidhaa zinazozalishwa

na Makampuni ya dawa katika jimbo hilo.

 

Maeneo mengine ni kubadilishana watumishi, semina za pamoja za wataalamu

wao katika nyanja mbalimbali, kubadilishana na kupeana taarifa za uwekezaji

kwenye sekta ya dawa, msaada wa kitaalamu na wataalam.

 

Mheshimiwa Majaliwa alimueleza Gavana huyo kuwa, kutokana na mpango

wa Serikali wa kuendelea kuimarisha eneo la utoaji huduma za afya, Serikali

ya Tanzania inawakaribisha wawekezaji kwa ajili ya kujenga viwanda vya dawa

na vifaa tiba ili kuwezesha upatikanaji rahisi wa dawa na vifaa tiba.

 

MSD Yapokea Shehena ya Vipimo vya UKIMWI na Kaswende

MSD-2.jpeg

 

Vipimo vya UKIMWI na Kaswende Vikiwa Vimepokelewa Ghalani Tayari kwa Usambazaji

 

 

DAR-ES-SALAAM

 

Katika kuadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani MSD imeendelea kupokea na kusambaza bidhaa mbalimbali za afya za kupambana na kudhibiti maambukizi ya Virusi vya UKIMWI Pamoja na Kaswende.

 

Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai ameeleza kuwa miongoni mwa bidhaa za afya ambazo kwa sasa inauhitaji mkubwa na inaendelea kusambazwa na MSD kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ni vipimo vya kupima maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na gonjwa la zinaa la Kaswende (HIV/ Syphilis Duo).

 

Vipimo hivyo vinafadhiliwa na Mfuko wa Dunia wa kupambana UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria  (The Global Fund) na pia hutumika kupima akina mama wajawazito kutambua maambukizi ya magonjwa yote mawili kwa wakati mmoja.

 

Kwa mujibu wa Dr. Ibadi Kaondo wa MSD, vipimo hivyo vinamsaidia mama mjamzito kutambua hali ya afya mapema, na endapo maambukizi yamegundulika inarahisisha kuanza matibabu mapema ili kufubaza makali ya virusi vya ukimwi na kutibu kaswende kwa ajili kuimarisha afya ya mzazi na kumkinga mtoto dhidi ya Maambukizi ya VVU, Kaswende ama kujifungua mtoto mfu.

 

Hapo awali vipimo hivi kila kimoja kilikuwa kinajitegemea, ambapo vilitumia muda mrefu kutoa majibu.  MSD kwa sasa ina shehena ya kutosha ya vipimo hivyo ambavyo tayari baadhi vilishaanza kusambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

 

Maadhimisho ya kitaifa ya siku ya UKIMWI duniani kwa mwaka 2022, yamefanyika katika viwanja vya Ilulu Mkoani Lindi, yakihudhuriwa na viongozi na wadau mbalimbali huku mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Katibu Mtendaji SADC Atembelea MSD

WhatsApp_Image_2022-10-26_at_16.08.41.jpeg

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  Mhe. Elias Mpedi Magosi (watatu kushoto) na Wajumbe Alioambatana Nao, Wakiwa Kwenye Picha ya Pamoja na Baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Bohari ya Dawa (MSD), Mara Baada ya Kutembelea Ofisi za Bohari hiyo, Zilizoko Keko, jijini Dar es Salaam

  

DAR ES SALAAM: 

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  Mhe. Elias Mpedi Magosi

pamoja na ujumbe wake, wametembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD), yaliyoko

Keko jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujionea jinsi taasisi hiyo inavyotekeleza majukumu

yake sambamba na kupokea mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa

manununzi ya pamoja (SPPS) kwaajili ya nchi wanachana.

 

Akizungumza kwa  niaba ya Menejimenti ya Bohari ya Dawa, Kaimu Mkurgenzi Mkuu

wa Bohari hiyo Bw. Leopold Shayo amempongeza Katibu Mtendaji huyo wa SADC

kwa kuzuru Tanzania, na hasa kuitembelea MSD, huku pia akianisha mafanikio

mbalimbali yaliyopatikana katika Jumuiya hiyo kupitia utekelezaji wa mpango

wa manunuzi ya pamoja kwa nchi wananchama.


Bw. Shayo amesema kwamba hadi kufikia sasa, MSD kupitia manunuzi ya pamoja

kwa nchi za SADC (SPPS) imewezesha kuundwa kwa Miongozo ya SPPS na

Mfumo wa Usimamizi wa mnyororo wa Ugavi kwa nchi wanachama, kuitisha

na kuendesha mkutano wa kitaalamu wa SADC Pooled Procurement wa kikanda

ili kuwezesha kubadilishana taarifa.

 

Ameongeza kwamba hadi sasa MSD imeweza kutengeneza mfumo kielektroniki

(e-SPPS) ili kusaidia kushughulikia miamala yote ya usimamizi wa ugavi wa

SPPS ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, ambamba na

kuwezesha kusainiwa kwa mikataba 41 na watengenezaji wa bidhaa za afya.

 

Aidha, Bw. Shayo amesisitiza kwamba MSD imewezesha kukuza uelewa juu

ya matumizi ya mfummo wa SPPS kwa kufanya mikutano na Mabalozi wa SADC

walioidhinishwa na Tanzania na nchi za SADC, ambapo hadi kufikia Februari

2022, nchi tatu (3) Wanachama zilikuwa zimeanza kutumia mfumo wa SPPS,

ambazo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Comoro, na Seychelles huku

zikiokoa kati ya 35% -70% ya gharama za unununzi wa bidhaa za afya.

 

Katika hatua nyingne nchi tatu (3) zaidi ambazo ni wanachama wa Jumuiya

hiyo ambazo ni Msumbiji, Malawi na Botswana zimeonyesha nia na utayari

wa kutumia jukwaa la SPPS, kutokana na mafanikio yaliyopatikana kupitia

mfumo huo wa manunuzi ya pamoja.

 

Naye kaimu Mkurugenzi wa Lojistiki wa MSD, Bw. William Singano, amesema

mbali na mafanikio yaliyopatikana kupitia mfumo huo wa manunuzi ya pamoja,

bado kuna uhitaji wa msukumo kwa nchi wanachama kutumia mfumo huo ili

kuwezesha lengo mahususi la uanzishwaji wa ushirikiano huo kutimia.

 

Bw. Singano ameuomba uongozi huo wa SADC, kusaidia upatikanaji wa taarifa

za kikanda za wazalishaji wa ndani, walioko ndani ya jumuiya, hatua itayosaidia

kuwawezesha kushiriki katika manunuzi ya bidhaa za afya na kuongeza pato na

ajira kwa nchi wanachama.

 

Aidha ameuomba uongozi huo wa SADC, kusaidia upatikanaji wa watu

mahususi (conctact person) kutoka nchi wanachama watakao kuwa wakisimamia

mfumo na taarifa zinazohusiana na SPPS.  Sambamba na hilo ameuomba uongozi

huo kusaidia upatikanaji wa orodha mahsusi ya bidhaa muhimu za afya 83, pamoja

na wazalishaji ili kusiaidia katika mipango ya manunuzi na uzalishaji.

 

Kwa upande wake Katibu wa SADC  Mhe. Elias Mpedi Magosi ameeleza kuwa

Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa nchi za Ukanda wa SADC ni

heshima kubwa kwa Taifa, kuaminiwa kwa huduma bora, uwezo na kukidhi

vigezo vya kitaalamu katika mnyororo wa ugavi. 

 

Ameupongeza uongozi wa MSD kwa hatua kubwa uliopiga katika mpango

wa manunuzi ya pamoja, huku akiahidi kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali

zilizowasilishwa na MSD, ili kuleta tija na msukumo wa manunuzi ya pamoja ya

bidhaa za afya kwa nchi wanachama.

 

Hatahivyo; ameitaka MSD kuongeza nguvu na ubunifu ili kuvutia nchi nyingi

zaidi na kuhakikisha kwamba lengo linafikiwa, huku akipongeza mpango wa

kutoa kipaumbele kwa wazalishaji wa ndani, kwani utainua uchumi wa nchi

wanachama pamoja na kuongeza ajira.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker