MSD Yapongezwa kwa Mageuzi ya Huduma, ndani ya Muda Mfupi.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_10.10.34.jpegMganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makorora mkoani Tanga, Dkt.Angelina Meshack, Akiongea na Waandishi na Ujumbe Maalum Kutoka MSD (Hawapo Pichani) Walipomtembelea Ofisini Kwake, Kupata Mrejesho wa Huduma Zitolewazo na Bohari ya Dawa (MSD)

 

TANGA:

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makorora mkoani Tanga, Dkt.Angelina Meshack

ameipongeza serikali kupitia MSD, baada ya kupokea vifaa vya chumba cha

upasuaji ikiwemo kitanda cha upasuaji, mashine ya dawa ya usingizi na taa

zinazotumika wakati wa upasuaji amesema vifaa hivyo ni msaada mkubwa

katika kituo hicho kwani awali kulikuwa na changamoto kwenye hutoaji huduma.

 

"Awali tulikuwa hatufanyi upasuaji kabisa kwa hiyo tulivyopokea fedha

kwa ajili ya ukarabati majengo ya kufanyia upasuaji tulifanya hivyo na

baadae vifaa vililetwa na MSD na kuanza kutoa huduma za upasuaji".

Amesema Dkt.Angelina

 

Amesema baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo walianza kutoa huduma ya

upasuaji mbalimbali wa mama wajawazito pamoja na upasuaji mdogo

kwani hapo awali walikuwa wanawapeleka wagonjwa hospitali ya Bombo

kwa sababu huduma hiyo haikuwepo hapo kituoni.



"Kwa ujio wa vifaa hivi imerahisisha mama mjamzito akipata changamoto

moja kwa moja tunaweza kumpa huduma ya upasuaji na tunaokoa

maisha ya mama pamoja na kichanga". Amesema.

 

Pamoja na hayo Dkt.Angelina amesema walikabidhiwa pia na jenereta kwa ajili

ya hospitali hiyo lakini wakaamua kuwasiliana na ofisi ya mganga mkuu ili

waweze kuichukua na kuikabidhi kwenye vituo vingine ambavyo havina jenerata

kwa sababu kituo hicho kilikuwa na jenerata ambayo walikuwa wameshanunua awali.

 

Ameeleza kuwa hali ya upatikanaji wa dawa katika kituo hicho ni nzuri kwani

kwa sasa dawa muhimu zinapatikana kwa asilimia 90 na wanaendelea kutoa

huduma bora kwa wananchi

                                    

 

Kamati ya Afya Bunge la Zambia, Yaipongeza MSD kwa Maboresho ya Utendaji na Ujenzi wa Viwanda

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_14.21.00.jpeg

Kamati ya Bunge ya Afya, Maendeleo na Huduma za Jamii ya Bunge la Zambia Ikiwa kwenye Ziara ya Kutembelea Viwanda vya MSD.

 

 DAR ES SALAAM:

Kamati ya Bunge ya Afya, Maendeleo na Huduma za Jamii,ya Bunge la Zambia

wamevutiwa na hatua ya Bohari ya dawa (MSD) kuanza kuzalisha baadhi ya

bidhaa za afya kwa kutumia wataalam wake wa ndani.

Hayo yamebainishwa hii leo, tarehe 26/5/2022 baada ya Kamati hiyo ya Afya

kutoka Zambia, kuitembelea MSD kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu

katika masuala yanayohusu mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_14.20.28.jpeg

Akizungumza kwaniaba ya ujumbe huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge ya Afya,

Maendeleo na Huduma za Jamii, ya Bunge la Zambia, Mhe.Dkt. Christopher K. Kalila

amesema wamevutiwa na hatua ya Bohari ya dawa (MSD) kuanza kuzalisha baadhi

ya bidhaa za afya kwa kutumia wataalam wake wa ndani.

 

Mhe.Dkt. Kalila ameongeza kuwa MSD Tanzania ni kama pacha wa Bohari ya Dawa

ya nchini Zambia, kwani sheria yao pia imefanyiwa mabadiliko na kuiwezesha Bohari

hiyo kuanza kuzalisha bidhaa za afya.

 

"Ni vyema taasisi zetu hizi mbili zikawa karibu ili kubadilishana uzoefu, na utaalamu

katika maeneo mabalimbali ili kusukuma kwa pamoja ajenda ya uanzishaji wa viwanda

vya bidhaa za afya na kuondoa utegemezi wa bidhaa kutoka nje sambamba na kupunguza

gharama." Alisema Dkt. Kalila.

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_14.20.27.jpeg

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai amesema

kwa pamoja na nchi nyingine kama Zambia yanaweza kufanyika mazungumzo

ya pamoja ya kuwezesha ununuzi wa pamoja wa bidhaa za afya, kupitia mpango

wa manunuzi ya pamoja ya SADC unaoratibiwa na MSD kwa nchi 16, kwa

kupitia mpango huo, nchi wanachama zitanufaika, sambamba na kupaisha soko

la viwanda vya ndani.

 

Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na mambo mengine wametembelea viwanda vya

MSD vya kuzalisha barakoa, pamoja na kiwanda cha dawa cha Keko Pharmaceuticals,

kinachosimamiwa na MSD.

                                              

 

MSD,Waganga Wakuu Mikoa na Wilaya Wajadili Upatikanaji Dawa Nchini

msasi_1.jpg

Mfamasia Mkuu wa Serikali Daud Msasi, Akihutubia Wakati wa Kikao Kazi Kati ya MSD na Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya Kilichofanyika Mkoani Dodoma.

           

                                         Mfamasia Mkuu wa Serikali Daud Msasi amewashauri 

                                         Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuunga Mkono

                                         juhudi za MSD kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya

                                    maabara, hatua ambayo itapunguza gharama za matibabu.

 

                                     Msasi amesema hayo kwenye kikao kazi cha MSD  na

                                   Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya uliofanyika Mkoani

                                                                      Dodoma.

 

                                Pia amewashauri MSD kuendeleza vikao vya aina hii kikanda,

                                  ili kujadiliana kwa kina namna ya kuboresha huduma, kwa

                                kuwa vikao hivi vinawakutanisha wataalamu mbalimbali ikiwa

                                     ni pamoja na wafamasia na wataalamu wa maabara.

msasi_3.jpg

Baadhi ya Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya Wakisilikiza Mada, Wakati wa Kikao Kazi Kati Yao na MSD Kilichofanyika Mkoani Dodoma.                              

                              

                               Kwa upande wake mwakilishi wa Waganga wakuu wa mikoa

                              Dkt. Japhet Simeo amewashauri waganga wakuu wa mikoa na

                                wilaya kutoa ushirikiano wa karibu kwa MSD ili kuboresha

                                                mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya.

 

 

 

                                 Amesema wakati huu ambapo MSD imekuja na mikakati

                                    mipya ya kuzalisha dawa na vifaa tiba ili kuwezesha

                                kupunguza gharama za bidhaa za afya, wao kama wataalam

                                            wawe washauri na waunge mkono juhudi hizo.

washima.jpg

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD Ndugu. James Washima, Akihutubia kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Wakati wa Kikao Kazi Kati ya MSD na Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya Kilichofanyika Mkoani Dodoma.

                                   

                                   Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD 

                                     Ndugu James Washima amesema kupitia Mkutano

                                      huu MSD inategemea kupata mrejesho mkubwa

                                        wa huduma inazozitoa kwa vituo vya kutolea

                                                     huduma za afya nchini.

 

 

 

 

                                                       “Tunawahakikishia kuwa

                                         tutachukua ushauri, maoni na changamoto

                                   mtakazotupatia na kuzifanyia kazi”. Alisema Washima

 

                         Amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Mhidze

                        na watendaji wote wa MSD  kwa maono yao ya kuanzisha viwanda vya

                        kuzalisha dawa na vifaa tiba kwani ununuzi bidhaa hizo kutoka nje ya nchi

                      na kwingineko  umekuwa ukiigharimu serikali fedha nyingi ambazo zingeweza

                                                   kutumika kuboresha huduma nyingine.

msasi_2.jpg

Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya Wakifuatilia Mada Wakati wa Kikao Kazi, Kati Yao na MSD Kilichofanyika Mkoani Dodoma.


                    

 

                          “Kamati yetu imesikia changamoto kutoka kwenu zinazowakwamisha kusonga

                          mbele, tunazichukua na kuzifikisha serikalini ili kuhakikisha MSD inaimarika

                            ipasavyo ili kuwezesha upatikanaji wa dawa nchini".Alisisitiza Washima

 


               

Mkurugenzi Mkuu MSD, Afanya Mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu PPRA

WhatsApp_Image_2022-08-19_at_13.55.37.jpeg

Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai, Akiteta jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA) Bw. Eliakim Maswi,Wakati Alipotembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD) kwa Lengo la Kubadilishana Mawazo.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Bw. Mavere Ali Tukai, amefanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) Bw. Eliakim C. Maswi, juu ya namna bora ya kuboresha ununuzi wa bidhaa za afya, kufuatia changamoto kadhaa zinazoikabili Bohari ya Dawa kwenye eneo hilo.

 

Mavere amemuelezea Afisa Mtendaji Mkuu huyo mtazamo wake juu ya ununuzi kwenye nyanja mbalimbali kama vile sheria, taratibu, miongozo pamoja na mfumo wa TANEPS.

 

Kupitia kikao hicho Mavere amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili Bohari ya Dawa upande wa ununuzi, na namna bora ya kuzitatua, ili kuboresha hali ya upatikanaji wa Dawa na Vifaa tiba nchini.

 

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu PPRA, amempongeza Bw. Mavere kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo, huku akiahidi kufanyia kazi kwa haraka, changamoto mbalimbali za kimanunuzi zinazoikabili MSD.

 

Aidha, amesisitiza taasisi za umma zimetofautiana upande wa mahitaji, hivyo kuahidi kuangazia na kutatua changamoto zilizobainishwa ili kuboresha manunuzi ya umma.

 

 

                                              

 

 

 

MSD Yapongezwa Ujenzi Viwanda vya Dawa na Vifaa Tiba

viwanda_-1.jpg

Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Mhidze akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Wakati Kamati hiyo Ilipotembelea Makao Makuu ya Bohari Hiyo,    yaliko Keko jijini Dar es Salam.

 

                         Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Mhe.  Daniel Sillo,

                           ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) kwa jitihada kubwa inazozizifanya

                         kuboreshaji upatikanaji wa bidhaa za afya nchini kwa kuanzisha viwanda

                         vya kuzalisha dawa na kuboresha viwanda vya dawa vilivyokuwa na hali

                                                                         mbaya.

 

                        Sillo ametoa pongezi hizo leo, Kamati hiyo ilipokuwa ziarani MSD, ambapo

                       pamoja na mambo mengine wajumbe wa Kamati hiyo  walitembelea kiwanda

                         cha dawa cha Keko, kiwanda cha MSD cha kuzalisha Barakoa pamoja na

                                  Maghala ya kuhifadhia bidhaa za afya dawa yaliyopo keko.

 

viwanda_-_2.jpg

 Msimamizi wa Kiwanda cha Kuzalisha Barakoa cha MSD, Bw. Twahil Magoolo akitoa maelezo juu ya uzalishaji Barakoa mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Wakati Kamati hiyo Ilipotembelea kiwandani hapo

 

                         Amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Mhidze

                        na watendaji wote wa MSD  kwa maono yao ya kuanzisha viwanda vya

                        kuzalisha dawa na vifaa tiba kwani ununuzi bidhaa hizo kutoka nje ya nchi

                      na kwingineko  umekuwa ukiigharimu serikali fedha nyingi ambazo zingeweza

                                                   kutumika kuboresha huduma nyingine.

 


                     “Kamati yetu imesikia changamoto kutoka kwenu zinazowakwamisha kusonga

                      mbele, tunazichukua na kuzifikisha serikalini ili kuhakikisha MSD inaimarika

                                      ipasavyo ili kuwezesha upatikanaji wa dawa nchini".

 

viwanda_-_4.jpg

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Wakipokea Maelezo kuhusu dawa, kutoka kwa Msimamizi ya Kiwanda cha Dawa cha Keko, Bi. Bettia Kaema.

 

                Naye Mkurugenzi Mkuu  wa MSD Meja Jenerali Gabriel Mhidze katika taarifa

                yake ya utendaji aliyoiwasilisha kwa Kamati hiyo ameeleza kuwa  pamoja

               na changamoto mbalimbali zinazoikabili MSD bado inaendelea kutoa huduma

                bora na za kiwango cha juu kwa wananchi na kusimamia mnyororo wa ugavi,

                                        ili kuleta tija kwenye mfumo wa afya wa nchi.

                


viwanda_-3.jpg

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Wakati Kamati hiyo Ilipotembelea Makao Makuu ya MSD, jijini Dar es Salaam

N

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker