MSD NA WADAU WA AFYA WAASWA KUZINGATIA WAJIBU KATIKA JAMII

WhatsApp_Image_2023-06-17_at_17.57.04.jpegKatibu Tawala Mkoa wa Mara, Bw. Masarika Robert Makungu, Akifungua Kikao Kazi Baina ya MSD Kanda ya Mwanza na Wadau Wake Kutoka Mkoa wa Mara, Kilichofanyika Jijini Mwanza.

Mwanza.

Wadau wa afya Mkoa wa Mara pamoja na Bohari ya Dawa (MSD) wametakiwa kuzingatia wajibu wao katika jamii, kwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi  na kuwa sehemu ya mabadiliko kwa kutoa huduma bora za afya, ili kuunga mkono kwa vitendo, juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuboresha huduma za afya nchini.

 

Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Bw. Masarika Robert Makungu, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD Kanda ya Mwanza na Wadau wake kilichofanyika jijini Mwanza kwa lengo la kujadili namna ya kuboresha mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya nchini.

 

Bw. Makungu ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza fedha za kutosha kwenye sekta ya afya, kwa lengo la kuboresha afya za wananchi na kuongeza nguvu kazi ya taifa, hivyo ni lazima kuwe na matokeo chanya na yenye tija kupitia watendaji.

 

"Kikao hiki kitatoa nafasi kwa watendaji kuchakata, kujadili na kupata suluhu ya ukosefu wa baadhi bidhaa za afya, hasa vifaa tiba na mwisho kuja na mapendekezo yatakayosaidia kuhakikisha tija kubwa inaonekana katika uwekezaji mkubwa ambao serikali ya Awamu ya Sita imefanya". Alisema Bw. Makungu.

 

Sambamba na hilo ameipongeza MSD kwa maboresho mbalimbali ambayo imekua ikiyafanya ikiwemo kupunguza muda wa kusubiri bidhaa.

Hata hivyo, Bw. Makungu amewataka wadau hao wa afya Mkoani humo kufanya maoteo sahihi ya bidhaa za afya ili kuipa ahueni MSD katika kuihudumia jamii.

 

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Zabron Masatu amesema wamejipanga kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa za afya unaimarika, hivo kikao hicho kimekuja wakati muafaka, kwani serikali imewekeza fedha za kutosha kwenye sekta ya afya Mkoani humo.

 

Aidha amepongeza MSD kwa kurudisha vikao vya wadau ili kuwekana sawa, huku akiahidi kusimamia kikamilifu masuala mbalimbali, ikiwemo maoteo suala ambalo limeonekana ni changamoto kupitia kikao hicho.

 

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Mwanza, Bw. Egidius Rwezaura amewashukuru wajumbe hao kwa muitikio wao, huku akibainisha maboresho mbalimbali yanayofanywa na MSD kwa sasa ikiwemo maboresho ya mfumo wa usambazaji, mikataba ya muda mrefu kwa wazalishaji na washitiri, uanzishaji wa viwanda vya bidhaa za afya, maboresho ya huduma, sambamba na rasilimali watu.

Wananchi Wahimizwa Matumizi Sahihi ya Vyandarua

WhatsApp_Image_2023-06-17_at_17.17.44.jpegMkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Remidius M. Emmanuel (kushoto), Akiteta Jambo na Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma Bw. John Sipendi na Ujumbe Wake mara Baada ya Kutembelea Ofisini Kwake 

Dodoma.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius M. Emmanuel amewataka wakazi na wazazi wote wilayani humo kutumia vyema na kwa lengo lililokusudiwa vyandarua vya msaada wanavyopatiwa serikali, ili adhima ya serikali ya kupambana na ugonjwa wa Malaria iweze kutimia.

Mhe. Remidius ametoa rai hiyo hii leo wakati akizindua rasmi zoezi la usambazaji wa vyandarua mashuleni wilayani humo, linalofanya na Bohari ya Dawa (MSD).

"lengo serikali kuwagawia vyandarua ni kuwakinga watoto wetu dhidi ya ugonjwa hatari wa Malaria, hivyo naomba vitumike kama ilivyokusudiwa na kwa matumizi ambayo ni kinyume na matakwa ya lengo la serikali kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria. Alisema Mhe. Remidius.

Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma, Bw. John Sipendi amesema MSD imejipanga vizuri kusambaza vyandarua kwenye shule zote zilizoainishwa na kwa muda uliopangwa.

" Sisi kama MSD tumejipanga kuhakikisha tunatekeleza zoezi hili la usambazaji kwa ufanisi na kwa wakati, hivyo niwatoe hof kwani hakuna shule itakosa vyandarua.

Bw. Sipendi ameongeza kuwa tayari magari ya usambazaji yako wilayani humo, na jumla ya vyandarua 87,038 vitasambazwa kwenye shule za msingi 123.

MSD Yapongezwa Kukutana na Wadau Wake

IMG-20230429-WA0155.jpg

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Ally Senga Gugu(katikati), Akiwa kwenye Picha ya Pamoja na Baadhi ya Watumishi wa Sekta ya Afya Mkoani humo, Wakati wa Kikao chan Wadau wa MSD.

 

Dodoma.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Ally Senga Gugu, ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dodoma kwa kukutana na wadau wake na kujadili masuala mbalimbali yahusuyo mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, yanayogusa pande zote mbili kwa lengo la kuboresha huduma na kuleta tija kwa wananchi. 

 

Mhe. Gugu ametoa pongezi hizo hii leo, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD Kanda ya Dodoma na wadau wake wa Mkoa wa Dodoma, kilichofanyika wilayani Kondoa, kwa lengo la kujadili mafanikio, maboresho na changamoto mbalimbali zilizopo baina ya pande hizo mbili.

 

Bw. Gugu ameongeza kuwa mkutano huo ni daraja muhimu la kuhakikisha MSD na wadau wake wanadumisha umoja ambao utawawezesha kuwahudumia wananchi kwa wakati, kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake, sambamba na kupokea changamoto zitakazoibuliwa na kuzipatia tatuzi ili kuboresha huduma za afya.

 

“Hakikisheni kunakua na majadiliano yenye tija ya namna bora ya kufanya kazi kwa Pamoja ili kila mmoja aweze kutimiza wajibu wa kumhudumia mwananchi. Ni mategemeo yangu baada ya Mkutano huu tutaondoka na uelewa wa Pamoja na maadhimio, ambayo utekelezaji wake utaboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya na kuboresha huduma.”_ alisema Bw. Gugu.

 

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Best Magoma, amewataka madaktari na watalaamu wote waliohudhuria Mkutano huo, kujadili kwa uwazi changamoto mbalimbali zinazowakabili, ili kuimarisha mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, kwani suala hilo ni mtambuka linalohitaji juhudi za pamoja ili kuepuka lawama zisizo za lazima baina ya MSD na wadau wake.

 

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma, Bw. John Sipendi, amewashukuru wadau wake kwa kuitikia wito wa kushiriki mkutano huo, huku akianisha mikakati na maboresho mbalimbali inayotekelezwa na MSD kwa sasa, ili kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za afya. Aidha ameomba wadau hao kuendeleza mahusiano na mawasiliano wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao, ili kuongeza tija katika kuhudumia wananchi.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Atoa Rai kwa Watumishi wa Afya

WhatsApp_Image_2023-06-17_at_16.04.31.jpegKatibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Ally Fatma Mganga (Aliyesimama), Akihutubia Wakati wa Kikao cha MSD na Wadau Wake Kutoka Mkoa wa Singida.

Singida.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt.Fatma Mganga, ametoa rai kwa MSD na wataalamu wengine wa afya wakiwemo Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaboresha huduma kwenye maeneo yao, ikiwemo upatikanaji wa bidhaa za afya, ili kuwahudumia wananchi kwa utimilifu.

Dkt. Mganga ametoa rai hiyo leo, wakati akifungua kikao kazi baina ya MSD na Wadau wake, kilichofanyika Mkoani Singida.

Ameongeza kuwa serikali ya Awamu ya Sita imejenga vituo vingi vipya vya kutolea huduma za afya nchini na kuviongeza hadhi vingine, hivyo kazi kubwa kwa MSD ni kuhakikisha bidhaa za afya hitajika katika vituo hivyo zinapatikana kwa wakati na huduma za afya zinatolewa kwa wananchi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victoria Ludovick, ameipongeza MSD kwa kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya Mkoani humo, ambapo kwa sasa umefikia asilimia 88%.

Hata hivyo, ameisihi MSD kuendelea kuboresha upatikanaji huo ili uwe maradufu, mathalani upatikanaji wa vifaa tiba.

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Dodoma. Bw. John Sipendi, amewashukuru wadau hao kwa kuitia mualiko huo, huku akihimiza umuhimu wa mijadala ya wazi ili kupata suluhu ya changamoto mbalimbali na hatimae kutoka na maazimio ambayo yatasaidia kuboresha huduma kwa pande zote mbili.

Mhe. Queen Sendiga Aipongeza MSD.

IMG-20230328-WA0112.jpgMkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhe. Queen Sendiga Akiwa Ofisini Kwake, Baada ya Kutembelewa na Ujumbe wa MSD.

 

Rukwa.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Sendiga amefurahishwa na huduma za MSD Mkoani humo na kusema kwamba hivi sasa huduma za afya hasa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarika kwa kiasi kikubwa.

Mhe. Sendiga ameongeza kuwa huduma na uhusiano wa MSD na Uongozi wa Mkoa wa Rukwa umeimarika na kwamba kero mbalimbali zilizokuwepo hapo awali, mathalani za upungufu wa bidhaa za afya sasa zimetatuliwa kwa kiasi kikubwa.

 “Ukienda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya unakuta dawa muhimu zinapatika kwa kiasi kikubwa, jambo linaloashiria kwamba MSD wameboresha huduma" alisema Sendiga.

Pamoja na kuboreka kwa huduma za MSD, Mkuu huyo wa Mkoa, ameiasa MSD kupitia Meneja wake wa kanda ya Mbeya Ndugu. Marco Masala, kutobweteka, bali kuhakikisha kuwa uboreshaji wa huduma uliopo sasa unakuwa endelevu ili wananchi waendelee kunufaika na huduma za MSD . 

Ameongeza kuwa zamani MSD ilikuwa inasemwa sana mitandaoni lakini kwasasa malalamiko yamepungua kwasababu huduma zimeendelea kuwa bora na za kutegemewa.

Kwaupande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya, Bw. Marco Masala ameahidi kuendelea kuboresha huduma, na kufanyia kazi changamoto mbalimbali zitazokuwa zikijitokeza ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker