MSD Yashiriki Mashindano ya Michezo ya SHIMIWI 2022
Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD), Wanaoshiriki kwenye Michezo ya Shimiwi 2022, wakiwa kwenye Maandamano Kuelekea Uwanaja wa Mkwakwani Jijini Tanga, Kwaajili ya Ufunguzi Rasmi wa Michuano hiyo.
TANGA: Bohari ya Dawa (MSD) inaendelea kushiriki Mashindano ya
Shirikisho la Michezo ya Wiraza na Idara za Serikali na
Mikoa (SHIMIWI) 2022, yanaendelea kupamba moto tangu
Oktoba 1, 2022 jijini Tanga, kwa michezo mbalimbali kutimua
vumbi ikiwemo mpira wa netiboli, mchezo wa kuvuta kamba
kwa wanaume na wanawake na mpira wa miguu, mbio za baiskeli,
michezo ya karata, riadha, bao na mingine mingi.
MSD inayowakilishwa na ujumbe wa wanamichezo 35,
imejiandikisha kushiriki michezo kadhaa, ikiwemo
kuvuta Kamba, netboli, mpira wa miguu, mbio za baiskeli,
riadha, mchezo wa karata na bao ili kuonyesha umahiri wao.
Mbali na kujiandikisha kushiriki michezo hiyo, wawakilishi wa MSD
pia walishiriki maandamano kwa kufanya matembezi kuelekea
uwanja wa Mkwakwani, kwaajili ya ufunguzi rasmi wa michezo hiyo.
Mgeni Rasmi katika ufunguzi huo, alikuwa ni Mhe. Jenista Mhagama
- Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, anayemuwakilisha Mhe. Waziri Mkuu.
Hatahivyo, baada ya ufunguzi huo rasmi, timu ya mpira wa miguu
ya MSD wanaume, imepangwa kufungua michuano hiyo kwa
kupepetana na timu ya Wizara ya Kilimo mbele ya Mgeni Rasmi.
|