MSD Yashiriki Mashindano ya Michezo ya SHIMIWI 2022

WhatsApp_Image_2022-10-05_at_12.23.37.jpeg

Watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD), Wanaoshiriki kwenye Michezo ya Shimiwi 2022, wakiwa kwenye Maandamano Kuelekea Uwanaja wa Mkwakwani Jijini Tanga, Kwaajili ya Ufunguzi Rasmi wa Michuano hiyo. 

  

TANGA: 

Bohari ya Dawa (MSD) inaendelea kushiriki Mashindano ya
 Shirikisho la Michezo ya Wiraza na Idara za Serikali na
Mikoa (SHIMIWI) 2022, yanaendelea kupamba moto tangu
Oktoba 1, 2022 jijini Tanga, kwa michezo mbalimbali kutimua
vumbi ikiwemo mpira wa netiboli, mchezo wa kuvuta kamba
kwa wanaume na wanawake na mpira wa miguu, mbio za baiskeli,
michezo ya karata, riadha, bao na mingine mingi.
 
MSD inayowakilishwa na ujumbe wa wanamichezo 35,
imejiandikisha kushiriki michezo kadhaa, ikiwemo
kuvuta Kamba, netboli, mpira wa miguu, mbio za baiskeli,
riadha, mchezo wa karata na bao ili kuonyesha umahiri wao.
 
Mbali na kujiandikisha kushiriki michezo hiyo, wawakilishi wa MSD
pia walishiriki maandamano kwa kufanya matembezi kuelekea
uwanja wa Mkwakwani, kwaajili ya ufunguzi rasmi wa michezo hiyo.
 
Mgeni Rasmi katika ufunguzi huo, alikuwa ni Mhe. Jenista Mhagama
- Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, anayemuwakilisha Mhe. Waziri Mkuu.
 
Hatahivyo, baada ya ufunguzi huo rasmi, timu ya mpira wa miguu
ya MSD wanaume, imepangwa kufungua michuano hiyo kwa
kupepetana na timu ya Wizara ya Kilimo mbele ya Mgeni Rasmi.

 

 

Serikali Ya Misri Yatoa Msaada wa Vifaa Tiba kwa Tanzania

WhatsApp_Image_2022-09-19_at_13.50.42.jpegBalozi wa Misri nchini Tanzania, Mhe. Mohamed Gaber Abuwafa (Kulia) Akikabidhi Msaada wa Vifaa Tiba kwa Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi(Kushoto), Makao Makuu ya Bohari ya Dawa, Jijini Dar es Salaam.

  

DAR ES SALAAM: 

Ubalozi wa Misri nchini Tanzania, leo tarehe 8/9/2022, umetoa

msaada vifaa tiba kwa Serikali ya Tanzania, kwa ajili ya kuboresha

huduma za afya nchini.

 

Vifaa hivyo vyenye thamani ya dola za Kimarekeni elfu 27 (USD 27,000),

ambazo ni sawa na takribani shilingi milioni 62.9 za kitanzania, umekabidhiwa

rasmi kwa serikali ya Tanzania.

 

Akikabidhi msaada huo Balozi wa Misri hapa nchini,

Mhe. Mohamed Gaber Abuwafa amesema serikali ya Misiri

itaendelea na juhudi za kuunga mkono serikali ya Tanzania

kuboresha huduma za afya.

 

"Serikali ya Misri kupitia shirika lake la EAPD, imetoa msaada huu

ili kuboresha huduma za afya, ikumbukwe huu sio msaada wa

kwanza na wala hautakua wa mwisho, kwani nchi zetu zimekua

na uhusiano wa muda mrefu katika nyanja mbalimbali,

hivyo mbali na msaada huu, tunatazamia siku zijazo

kuazisha ushirikiano katika kubadilishana utaalamu na

wataalamu kupitia sekta ya afya".

Alisisitiza Balozi Mhe. Abuwafa

 

Mhe. Abuwafa ameongeza kuwa Serikali ya Misri inaangalia

uwezekano wa kuwekeza nchini kwenye sekta ya viwanda

vya dawa na vifaa tiba, ili kuendeleza uhusiano wa muda

mrefu baina pande hizo mbili.

 

"Serikali ya Misri itaendela kusaidia sekta mbalimbali nchini,

ikiwemo uanzishaji wa viwanda vya dawa, ili kuunga mkono

juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha na

kusogeza huduma za afya karibu na jamiii kwa gharama nafuu"

Alisema Balozi Abuwafa.

 

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Serikali ya Tanzania,

Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi, ameishukuru Serikali

ya Misri kupitia ubalozi wake nchini, kwa kuipatia Tanzania

msaada huo, na kusisitiza kwamba utaenda kuwa chachu ya

kuboresha afya za wananchi.

 

"Kwa niaba ya serikali ya Tanzania, tunaipongeza na kuishukuru

serikali ya Misri kwa kutupatia msaada huu kwaajili ya kuboresha

afya za watanzania na ushirikiano uliopo baina ya mataifa yetu,

tunatumaini kwamba huu hautakuwa msaada wa mwisho,

bali muendelezo wa ushirikiano zaidi baina ya mataifa yetu."

Alisema Msasi

Dkt. Mollel Aishauri MSD Namna ya Kuboresha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya Nchini.

WhatsApp_Image_2022-09-01_at_08.10.55.jpegNaibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel Akiongea Watumishi wa MSD, Mara baada ya Kutembelea Banda lao, Wakati Maonesho ya Kimataifa ya Wadau wa Bidhaa za Afya ya Afrika Mashariki, Yanayofanyika Jijini Dar es Salaam.

 

 

  

DAR ES SALAAM: 

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameishauri Bohari ya Dawa (MSD)

kutengeneza mpango wa muda mrefu wa kuzungumza na wazalishaji dawa

na bidhaa nyingine za afya kutoka nchi zinazozalisha bidhaa hizo, ili

kuja kuwekeza nchini Tanzania, hatua ambayo itarahisisha upatikanaji

wa bidhaa za afya nchini.

 

 

Naibu waziri ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa maonesho ya

Kimataifa ya wadau wa bidhaa za afya ya Afrika Mashariki

yaliyoanza leo jijini Dar es Salaam.

 

 

Ameongeza kuwa MSD pia iangalie namna ya kuingia mikataba na nchi

zinazozalisha bidhaa za afya kurahisisha kununua moja kwa moja kutoka

kwao, ili kupunguza gharama na kuwezesha kupata bidhaa za

kutosheleza mahitaji.

 

 

Kiongozi huyo pia amewahimiza wazalishaji hao wa nje kuja kuwekeza nchini

Tanzania kwa kuingia ubia na serikali.

 

 

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano MSD Bi. Etty Kusiluka,

 amemshukuru Dkt. Mollel kwa ushauri, na kuahidi kuufikisha kwenye Menejimenti ya

MSD ili uweze kufanyiwa kazi.

 

 

Aidha, ameendelea kuwakaribisha wananchi na wadau mbalimbali kutembelea banda la

MSD lilipo kwenye maonyesho hayo, ili waweze kupata taarifa mbalimbali

zinazohusiana na MSD, sambamba na kufahamu namna taasisi hiyo

inavyotekeleza majukumu yake.

 

 

Maonyesho hayo ya Kimataifa ya bidhaa za afya ya Afrika Mashariki yanafanyika

kwa siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee, ulioko jijini Dar es Salaam,

kwa kuwakutanisha Wadau kutoka nchi mbalimbali.

MSD Yatoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Vifaa Tiba na Maabara Nchini.

WhatsApp_Image_2022-09-19_at_13.26.53.jpegKaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa MSD Bw.William Singano, Akiongea na Wataalamu wa Vifaa Tiba na Mabaara nchini, Wakati wa Kufunga Mafunzo, yaliyoendeshwa na MSD kwa Wataalamu Mkoani Morogoro.

  

Morogoro: 

Mafunzo ya siku tatu kwa wahandisi vifaa tiba na wataalam wa Maabara

nchini, yamefungwa leo mkoani Morogoro.

 

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa wakati mmoja kwa mikoa mitano kwa ajili ya wataalam

wa nchi nzima yalikuwa na lengo la kuwafundisha wataalamu wa usimikaji,

matumizi na ukarabati wa mashine za maabara na vifaa vinavyosambazwa

na MSD.

 

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD,

Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji Bw.William Singano amesema

mafunzo hayo ni muhimu kwa wahandisi vifaa tiba na wataalam wa maabara

kwa kuwa yanawawesha watumiaji hao kumudu kuzitumia, kuzitunza na

kuzifanyia ukarabati.

 

BW. Singano ameishuikuru Serikali kuboresha huduma za afya kwa kuwezesha

mashine na vifaa vya kisasa nchi nzima.

 

Mafunzo hayo yalitolewa mikoa ya Tabora, Morogoro, Mbeya, Kilimanjaro

na Mwanza ambapo wataalam kutoka mikoa mingine yote waliungana

kupata mafunzo hayo kwa pamoja.

MSD Yachangia Maboresho ya Huduma za Uzazi Visiwani Zanzibar

WhatsApp_Image_2022-08-30_at_09.45.30.jpeg

Kaimu Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam Bw. Nuru Mwagoka,Akipokea Cheti Kutoka Kwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar     Mhe. Dkt. Husein Ally Mwinyi Kufuatia Mchango MSD Kwenye Mbio za Hisani Zilizolenga Kuboresha Huduma za Uzazi

 

  

ZANZIBAR:

Bohari ya Dawa (MSD), imeshiriki mbio na matembezi
ya hisani kwa ajili kuchangia huduma za uzazi salama kwa mama
na mtoto, zilizoandaliwa na Shirika la AMREF,
visiwani Zanzibar.
 
Akizungumza wakati wa kuhitimisha mbio hizo zilizoanzia
viwanja wa Maisara- Mnazi Mmoja majira ya asubuhi,
Mgeni Rasmi wa Shughuli hiyo, Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Husein Ally Mwinyi,
amewapongeza washiriki wote ikiwemo MSD kwa kushiriki
tukio hilo la kihistoria kuchangia maboresho ya huduma za
uzazi salama visiwani humo.
 
WhatsApp_Image_2022-08-30_at_09.45.29.jpeg 
“Nawapongeza wananchi, makampuni na mashirika wote
kwa ujumla kwa kushiriki kwenu kwenye mbio hizi za kusaidia
huduma ya mama na mtoto". Alisema Dkt. Mwinyi. 
 
Rais Mwinyi ametoa wito kwa taasisi, makampuni na wadau
mbalimbali kuiga mfano wa AMREF, ili kusaidia huduma
mbalimbali visiwani humo.
 
Ameongeza kwamba Serikali yake itaendelea kushirikiana
kwa ukaribu na wadau wote wenye nia ya kuchangia
maendeleo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Kaimu
Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam, Bw. Nuru Mwangoka,
amesema MSD ni mdau wa karibu kwa serikali ya mapinduzi
ya Zanzibar hasa kupitia sekta ya afya, hivyo walivyopokea
wito wa kushiriki na kuchangia huduma za afya hawakusita
kufanya hivyo.
WhatsApp_Image_2022-08-30_at_09.45.301.jpeg
 
"Sisi MSD, ni washirika muhimu wa sekta ya afya Zanzibar
kwani tumekua tukifanya kazi zetu kwa ushirikiano na Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, hivyo tulivyopokea wito wa
kushangia huduma hizi za uzazi hatukusita kushiriki”
alieleza Bw. Mwangoka
 
Aliongeza kuwa MSD kwenye mbio na matembezi hayo ya hisani,
imeweza kuchangia vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha
huduma za uzazi salama, visiwani humo.
 
Aidha, amesema msaada huo umekwisha wasilishwa kwa uongozi
wa AMREF, ukisubiri kupelekwa kwenye vituo vya kutolea
huduma za afya.
 
Katika mbio na matembezi hayo, washiriki wote wameweza
kutembea na kukimbia mbio hizo na kumaliza ikiwemo Kilometa 5,
na Kilometa 10, ambapo zote zimemalizikia katika viunga
vya uwanja wa Amaani.

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker