Katibu Mtendaji SADC Atembelea MSD

WhatsApp_Image_2022-10-26_at_16.08.41.jpeg

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  Mhe. Elias Mpedi Magosi (watatu kushoto) na Wajumbe Alioambatana Nao, Wakiwa Kwenye Picha ya Pamoja na Baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Bohari ya Dawa (MSD), Mara Baada ya Kutembelea Ofisi za Bohari hiyo, Zilizoko Keko, jijini Dar es Salaam

  

DAR ES SALAAM: 

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  Mhe. Elias Mpedi Magosi

pamoja na ujumbe wake, wametembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa (MSD), yaliyoko

Keko jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujionea jinsi taasisi hiyo inavyotekeleza majukumu

yake sambamba na kupokea mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa

manununzi ya pamoja (SPPS) kwaajili ya nchi wanachana.

 

Akizungumza kwa  niaba ya Menejimenti ya Bohari ya Dawa, Kaimu Mkurgenzi Mkuu

wa Bohari hiyo Bw. Leopold Shayo amempongeza Katibu Mtendaji huyo wa SADC

kwa kuzuru Tanzania, na hasa kuitembelea MSD, huku pia akianisha mafanikio

mbalimbali yaliyopatikana katika Jumuiya hiyo kupitia utekelezaji wa mpango

wa manunuzi ya pamoja kwa nchi wananchama.


Bw. Shayo amesema kwamba hadi kufikia sasa, MSD kupitia manunuzi ya pamoja

kwa nchi za SADC (SPPS) imewezesha kuundwa kwa Miongozo ya SPPS na

Mfumo wa Usimamizi wa mnyororo wa Ugavi kwa nchi wanachama, kuitisha

na kuendesha mkutano wa kitaalamu wa SADC Pooled Procurement wa kikanda

ili kuwezesha kubadilishana taarifa.

 

Ameongeza kwamba hadi sasa MSD imeweza kutengeneza mfumo kielektroniki

(e-SPPS) ili kusaidia kushughulikia miamala yote ya usimamizi wa ugavi wa

SPPS ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, ambamba na

kuwezesha kusainiwa kwa mikataba 41 na watengenezaji wa bidhaa za afya.

 

Aidha, Bw. Shayo amesisitiza kwamba MSD imewezesha kukuza uelewa juu

ya matumizi ya mfummo wa SPPS kwa kufanya mikutano na Mabalozi wa SADC

walioidhinishwa na Tanzania na nchi za SADC, ambapo hadi kufikia Februari

2022, nchi tatu (3) Wanachama zilikuwa zimeanza kutumia mfumo wa SPPS,

ambazo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Comoro, na Seychelles huku

zikiokoa kati ya 35% -70% ya gharama za unununzi wa bidhaa za afya.

 

Katika hatua nyingne nchi tatu (3) zaidi ambazo ni wanachama wa Jumuiya

hiyo ambazo ni Msumbiji, Malawi na Botswana zimeonyesha nia na utayari

wa kutumia jukwaa la SPPS, kutokana na mafanikio yaliyopatikana kupitia

mfumo huo wa manunuzi ya pamoja.

 

Naye kaimu Mkurugenzi wa Lojistiki wa MSD, Bw. William Singano, amesema

mbali na mafanikio yaliyopatikana kupitia mfumo huo wa manunuzi ya pamoja,

bado kuna uhitaji wa msukumo kwa nchi wanachama kutumia mfumo huo ili

kuwezesha lengo mahususi la uanzishwaji wa ushirikiano huo kutimia.

 

Bw. Singano ameuomba uongozi huo wa SADC, kusaidia upatikanaji wa taarifa

za kikanda za wazalishaji wa ndani, walioko ndani ya jumuiya, hatua itayosaidia

kuwawezesha kushiriki katika manunuzi ya bidhaa za afya na kuongeza pato na

ajira kwa nchi wanachama.

 

Aidha ameuomba uongozi huo wa SADC, kusaidia upatikanaji wa watu

mahususi (conctact person) kutoka nchi wanachama watakao kuwa wakisimamia

mfumo na taarifa zinazohusiana na SPPS.  Sambamba na hilo ameuomba uongozi

huo kusaidia upatikanaji wa orodha mahsusi ya bidhaa muhimu za afya 83, pamoja

na wazalishaji ili kusiaidia katika mipango ya manunuzi na uzalishaji.

 

Kwa upande wake Katibu wa SADC  Mhe. Elias Mpedi Magosi ameeleza kuwa

Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa nchi za Ukanda wa SADC ni

heshima kubwa kwa Taifa, kuaminiwa kwa huduma bora, uwezo na kukidhi

vigezo vya kitaalamu katika mnyororo wa ugavi. 

 

Ameupongeza uongozi wa MSD kwa hatua kubwa uliopiga katika mpango

wa manunuzi ya pamoja, huku akiahidi kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali

zilizowasilishwa na MSD, ili kuleta tija na msukumo wa manunuzi ya pamoja ya

bidhaa za afya kwa nchi wanachama.

 

Hatahivyo; ameitaka MSD kuongeza nguvu na ubunifu ili kuvutia nchi nyingi

zaidi na kuhakikisha kwamba lengo linafikiwa, huku akipongeza mpango wa

kutoa kipaumbele kwa wazalishaji wa ndani, kwani utainua uchumi wa nchi

wanachama pamoja na kuongeza ajira.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker