DKT. Shein Amwaga Pongezi kwa MSD.

DKT_SHEIN.jpg3.jpg

                          Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi

                    Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein ameipongeza MSD kwa kuteuliwa

                           kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa ajili ya nchi za SADC.

 

                                Dkt. Shein alimweleza hayo Mkurugenzi Mkuu wa MSD

                        Laurean Bwanakunu alipotembelea banda la MSD katika maonesho

                                  ya viwanda yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

 

                  Kingozi huyo pia ameishauri MSD kuwatembelea wazalishaji wakubwa

                       wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara wa mataifa

                     ili wapate taarifa sahihi na kuwashirikisha kuhusu MSD kuteuliwa

                        kusimamia manunuzi ya pamoja ya dawa kwa nchi za SADC.

 

                           DKT_SHEIN.jpg                               

                          

                     Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu

                   amesema tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya manunuzi ya pamoja,

                   ambapo tayari wameanza mchakato wa kupata wazabuni na kuanzisha

                mfumo wa kielektroniki utakaotumiwa na nchi wanachama kuleta mahitaji.

 

               Bohari ya Dawa MSD, ni moja ya taasisi zilizoshiriki maonyesho ya biashara

              na viwanda ya SADC yaliyofanyika wakati wa wiki ya mkutano wa SADC 2019,

                   katika viwanja vya kimataifa vya Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker