Waziri Ummy Mwalimu, Ahimiza Ujenzi wa Viwanda vya Dawa Nchini

5555555555.jpg

                                ,

 

        Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu

          amesema serikali inawajengea mazingira mazuri wazalishaji dawa,vifaa tiba na

     vitendanishi vya maabara wanaowekeza nchini kwani wanasaidia kupunguza gharama

                                                za kuagiza dawa nje ya nchi.

 

        Waziri Huyo ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa Tatu wa mwaka

        wa wazalishaji na wasambazaji Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi vya Maabara

                                       kutoka nchi mbalimbali duniani.

 

7777777777.jpg

 

            Mkutano huo umeandaliwa na Bohari ya Dawa kwa kushirikiana na UNDP

             ambapo mwakilishi wa UNDP Dr. Rosemary Kumwenda amesema mkutano

           huu ni muhimu kwani MSD kwa sasa inafanya kazi kimataifa na UNDP kama

             wakala wa maendeleo wa Umoja wa Mataifa inawajibu wa kuunga mkono

           jitiada za MSD kuhakikisha shughuli zinazofanywa na MSD zinakuwa na              

                                                  manufaa kwa wananchi.

 

6666666666666.jpg

 

           Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amesema wameandaa

               mkutano huo ili kuweka mazingira ya uwazi na kuboresha utendaji wa

         MSD na kuwavutia wazalishaji wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi vya Maabara

                                                        kuja kuwekeza.


 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker