Waziri Ummy Aipongeza MSD Kununua Dawa SADC

 

UMMY_SADC.jpg4.jpg

                   Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

              Mhe.Ummy Mwalimu (Mb) amesema hatua ya MSD kununua dawa

             za SADC itasaidia kupunguza gharama za kununua dawa kwa nchi

                            husika na kuboresha upatikanaji wa dawa.

 

                Ameeleza kuwa kwa nchi moja moja kununua dawa ni gharama,

              ndio maana serikali ya Tanzania kupitia MSD imeteuliwa kufanya

           manunuzi ya pamoja ya dawa kwa nchi hizo,na tayari wameshatangaza

                                                     zabuni.

 

                  Waziri huyo ameeleza hayo kwa waandishi alipotembelea banda

                     la MSD kwenye Maonesho ya wiki ya viwanda yanayoendelea

               jijini Dar es Salaam yanayoshirikisha wadau kutoka nchi mbalimbali

                                                    za Afrika.

 

               Maonesho ya viwanda ni utangulizi wa mkutano wa 39 wa SADC 2019,

                       ambao mwaka huu Tanzania ni mwenyeji wa mkutano huo .

 

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker