Siku ya wanawake

Wanawake wa MSD waliungana na wanawake wengine duniani kuadhimisha siku ya wanawake, ambapo walitumia siku hiyo kupata mada zinazohusu haiba ya utumishi pamoja na malezi na makuzi ya mtoto. Awali akifungua maadhimisho hayo, mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Dkt. Joseline Kaganda amewapa changamoto wanawake ya kujiendeleza kielimu, ili kuendana na kasi ya maendeleo, sayansi na teknolojia ulimwenguni.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa MSD Victoria Elangwa amesema hatua hiyo ya kuwapa mada wanawake imefanywa pia kwenye kanda zote nane (8) za MSD, Mada kuu ilikuwa kudhibiti msongo wa mawazo kazini (stress management at work place) na Kujikinga na magonjwa yanayowasumbua wanawake.

Amesema nia ya mada zote ni kuhakikisha wanawake wanakua na afya bora kimwili na kisaikolojia, ili kuwa imara wawapo kazini na kwenye jamii.Watoa mada walioshiriki siku hiyo ni pamoja na Grace Makani na Ester Simba.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker