Madereva wa MSD Wajengewa Uwezo

madereva-7.jpeg

Baadhi ya Watumishi wa MSD wa Kada ya Udereva, Wakiwa Mafunzoni Katika Chuo cha Chuo cha Ufundi Veta, Kilichoko Mkoani Morogoro, Walikokwenda Kuongeza Ujuzi wa Kuendesha Magari Makubwa ya Mizigo.

ARUSHA.

Watumishi wa MSD wa kada ya Udereva, wameendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo mbalimbali, yanayoandaliwa na taasisi mathalani udereva wa kujihami, alama za barabarani, ukaguzi wa magari, sheria za usalama barabarani, upakiaji wa mizigo na namna bora ya kuendesha magari makubwa yanayovuta tella (truck and trailers) ili kuongeza tija katika kazi zao na taasisi kwa ujumla.

Mafunzo hayo ya siku 10 yamehusisha nadharia na vitendo na yametolewa na wataalamu kutoka Chuo cha Ufundi Veta, kilichoko Mkoani Morogoro.

madereva_-2.jpeg

Kwaupande wake Mkufunzi wa Chuo hicho Bw. William Emmanuel Munuo, ambaye amekuwa akiendesha mafunzo hayo ameipongeza MSD kwa kuratibu mafunzo hayo, kwani yamekua na tija kwa wanafunzi wake.

"Teknolojia zinabadilika katika magari, alama za usalama zinaongezeka, barabara zinabadilika, hivi sasa nchini zipo barabara za juu na chini, hivyo ni vyema kuwanoa maderava wetu ili waweze kwenda na wakati, niwapongeze MSD kwa kuliona hilo" Alisema Bw.Mnuo

Akizumgumza kwaniaba ya Maderava wa MSD Bw. Marwa Wangwe, amesema mafunzo hayo yamewaongezea ujuzi, kujiamini na uelewa wa masuala mbalimbali ya muhimu katika uedenshaji wa vyombo vya moto.

madereva-1.jpeg

Aidha ameiomba Menejimenti ya MSD, kuratibu mafunzo hayo mara kwa mara, ili kuwajengea uwezo na kuongeza tija katika utekelezaji wa shughuli za taasisi

MSD Kilimanjaro Yajadili Mbinu Kuboresha Uhusiano na Huduma kwa Wateja

MOSHI.jpeg

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Vones Uisso, Akifungua Mkutano Baina ya MSD Kanda ya Kilimanajaro na Wateja Wake, Uliofanyika Jijini Arusha. 

 

ARUSHA.

 

MSD Kanda ya Kilimanjaro imekutana na wateja wake wanaopata huduma kutoka Kanda hiyo ambao ni kutoka mikoa yaArusha, Kilimanjaro na Manyara, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanagusa pande hizo, kwa lengo la kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi. 

 

Mkutano huo wa siku moja umefanyika Mkoani Arusha ukiwa na lengo la kujenga uhusiano mzuri baina ya MSD Kanda ya Kilimanjaro na wateja wake wote wanaohudumiwa na Kanda hiyo.

 

Akifungua Mkutano huo Kaimu mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bi. Vones Uisso, amesema mkutano huo utawawezeshaMSD kupokea maoni na ushauri utakaochangia kuboresha huduma ambazo wanazitoa kwa wateja wake.

Ameongeza kuwamkutano huu utawezesha MSD kujadiliana namna nzuri ya kufanya kazi kwa pamoja na wateja wake ili kila mmoja awezekutimiza wajibu wa kumhudumia mwananchi.

 

Kwa upande wake Meneja wa Kanda ya Kilimanjaro Bi. Rehema Shelukindo amesema mkutano huu wa wateja utadumishaumoja, ambao utaendelea kuwezesha kuwahudumia wananchi kwa wakati.

 

Ameongeza kuwa mkutano huo utawezeshakupokea maboresho ambayo wateja wanawasilisha na kuyafanyia kazi.

 

 

Kamati ya CCM Mkoa wa Njombe, Yatembelea Kiwanda cha MSD- Idofi

WhatsApp_Image_2023-02-06_at_15.10.15.jpeg

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe Mhe. Deo Sanga, Akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Antony Mtaka Pamoja wa Wananchi Wengine, Wakati Kamati ya CCM Mkoani Humo ilipotembelea Kiwanda cha Mipira ya Mikono cha MSD- Idofi, Kilichoko Makambako, Mkoani Njombe.

 

 

NJOMBE

Kamati ya CCM Mkoa wa Njombe ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe.Deo Sanga, Mbunge wa jimbo la Makambako, imetembelea na kukagua maendeleo ya Mradi wa Kiwanda cha mipira ya mikono, kilichoko Idofi Makambako.

 

Kamati hiyo iliyoongozana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka imeelezea kufurahishwa na hatua zilifikiwa katika ujenzi wa mradi huo na kuipongeza Menejimenti na Wataalamu wa MSD kwa kufanikisha ujenzi huo.

 

Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo, Mhe. Deo Sanga, ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha nyingi kwaajili ya ujenzi huo, kwani utasaidia taifa katika upatikanaji wa bidhaa za afya na kuokoa matumizi ya fedha za kigeni.

 

Mhe.Deo Sanga ameiomba serikali sikivu ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, kumalizia angwe ya ujezi iliyobakia, ambayo inakadiriwa kugharimu takribani Bilioni 5 ili kukamilisha mradi huo.

 

Aidha Mhe. Deo Sanga amewaasa wakazi wa Idofi kulinda mradi huo, sambamba na kutumia fursa za uwepo wa mradi huo kujiinua kiuchumi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Njombe amepongeza uwepo wa kiwanda hicho Idofi Makambako na kueleza kuwa mradi huo ni fahari kwa wana Njombe na Taifa kwa ujumla.

 

Kufuatia kiwanda hicho kuwa kwenye majaribio ya uzalishaji, wajumbe hao walipata sampuli za glavu za majaribio kwa ajili ya kuziweka ofisini kwao kama alama ya bidhaa inayozalishwa Mkoani kwao

MSD Kanda ya Mbeya, Yateta na Wafamasia Kuboresha Huduma

MBEYA_-2.jpeg

 

Wafamasia Wanaohudumiwa na Kanda ya Mbeya, Wakiwa Kwenye Picha ya Pamoja na Baadhi ya Watumishi wa MSD Kanda ya Mbeya. 

 
MBEYA:
MSD Kanda ya Mbeya imefanya kikao na wafamasia kutoka Halimshauri 17 na wafamasia wa mikoa yote inayoihudumia.
 
Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya Bw. Marco Masala amesema lengo la kikao hicho ni kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za upatikanaji wa bidhaa za afya katika mikoa hiyo, pamoja na kuimarisha uhusiano.
 
Pamoja na mambo mengine kupitia kikao hicho wamekubaliana kuunda kamati maalum ya kudumu itakayosaidiana na Kanda ya MSD Mbeya kufuatilia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa kwenye kikao hicho. 
 
 
Naye mwenyekiti mteule wa Kamati hiyo Bi. Lucia Mkumbo (Mfamasia wa Mkoa wa Mbeya) ameipongeza MSD kwa kufanikisha kikao hicho na kusema kuwa wapo tayari kufanya kazi kwa kushirikiana ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa, ikiwa ni pamoja na kusimamia na kuhakikisha kuwa vituo vya afya vinaleta maombi ya mahitaji yao mapema na kutumia vyanzo vingine vya mapato badala ya kutegemea fedha inayotoka Serikali kuu pekee.
 
 
 
Hivi karibuni MSD kupitia mipango yake mbalimbali, imejidhatiti kuhakikisha inaimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini, sambamba na kuboresha mawasiliano na mahusiano na wateja na wadau wake
 

 

 

MSD Yafuatilia Ubora wa Dawa-Vituoni

WhatsApp_Image_2023-02-06_at_16.27.20.jpeg

 

 

Bohari ya dawa (MSD) kupitia Kitengo chake cha Udhibiti Ubora imeendelea na zoezi la ufuatiliaji wa ubora wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ambavyo vimeshasambazwa kwa wateja ili kuhakikisha bidhaa hizo za afya hasa dawa, zinaendelea kuwa na ubora unaotakiwa.

 

Zoezi hili ni muongozo uliotolewa na Shirika la Afya duniani (WHO) pamoja na ushauri wa Mamlaka ya Dawa na vifaa tiba (TMDA) kuitaka MSD kama msambazaji wa bidhaa za afya nchini kufuatilia ubora wa bidhaa ambazo tayari zipo kwa wateja na kujionea jinsi zinavyotunzwa, ili kulinda afya za watumiaji kwani kumekuwepo na changamoto nyingi kwenye mnyororo wa ugavi wa dawa, zinazoweza kuathiri ubora wa awali wa dawa na vifaa tiba, ikiwemo namna ya usafirishaji, utunzaji na hali ya hewa kwenye maeneo yao.

 

Katika mwaka wa Fedha 2022/2023 tayari zoezi hili limeshafanyika katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Kilimanjaro na Tanga kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati, huku zoezi hilo likitarajiwa kuendelea kwenye mikoa mingine.

 

Zoezi hili hutekelezwa kila mwaka ili kulinda afya za watumiaji ikiwa ni pamoja na kushauri juu ya mapungufu yatakayoonekana katika vituo vya kutolea huduma za afya, ili kuepusha athari za ubora wa bidhaa hizo.

 

Zoezi hili huangazia namna ya usafirishaji, utunzaji na hali ya hewa kwenye maeneo ambapo bidhaa hizo huhifadhiwa katika vituo hivyo.

Lock full review www.8betting.co.uk 888 Bookmaker